JW subtitle extractor

Yehova Aliendelea Kuonyesha Upendo Mushikamanifu

Video Other languages Share text Share link Show times

Katika hii ulimwengu, sisi wote tunapata majaribu.
Uko hakika kama Yehova atakusaidia?
Kama ni vile, atakusaidia wakati gani?
Tunaweza kuwa hakika kama
Yehova atatusaidia wakati wa majaribu.
Juu ya nini?
Ni juu sifa kubwa ya Yehova ni upendo
sifa yenye kugusa moyo sana.
Ili tujifunze juu ya ile sifa,
na kujua namna tunaweza kuionyesha,
tuchunguze habari ya Biblia kuhusu Yosefu.
Yosefu alizaliwa Mesopotamia
kumepita zaidi ya miaka 3700.
Baba yake alikuwa Yakobo; na aliitwa pia Israeli.
Yosefu alikuwa na ndugu mumoja wa kweli, Benyamini;
na alikuwa na ndugu-nusu kumi.
Wakati alikuwa mudogo, Yosefu alianza kupata magumu,
juu ndugu zake kumi walimusikilia wivu.
Lakini, juu Yosefu alivumilia majaribu,
ile ilifanya aokoe familia yake yote isikufe na njaa;
na inatupatia nafasi ya kupata baraka za milele.
Nawaomba mufungue Biblia zenu
na tusome pamoja Mwanzo 37:2-11.
Wakati Yosefu alikuwa na miaka kumi na saba
alikuwa anachunga kundi pamoja na
wana wa Bilha na wana wa Zilpa,
bibi za baba yake.
Na Yosefu akamuletea baba yao
habari ya mubaya juu yao.
Sasa Israeli alimupenda Yosefu kuliko
wana wake wengine wote
kwa sababu alikuwa mwana wa uzee wake,
na alimushoneshea kanzu ya pekee.
Wakati ndugu zake waliona kwamba baba yao
alimupenda zaidi kuliko ndugu zake wote,
wakaanza kumuchukia na hawakukuwa
wanazungumuza naye kwa amani.
Kisha wakati fulani
Yosefu aliota ndoto na akaielezea ndugu zake,
na wakapata sababu ingine ya kumuchukia.
Aliwaambia:
Tafazali musikilize ndoto yenye niliota.
Tulikuwa tunafunga mafungu ya
nafaka katikati ya shamba,
halafu fungu langu la nafaka
likainuka na kusimama wima,
na mafungu yenu ya nafaka yakazunguka
na kuinamia fungu langu la nafaka.
Ndugu zake wakamuambia:
Je, kweli utajifanya kuwa mufalme
juu yetu na kututawala?
Kwa hiyo wakapata sababu ingine ya kumuchukia,
kwa sababu ya ndoto zake na mambo yenye alisema.
Kisha mambo hayo
akaota tena ndoto ingine,
na akaielezea ndugu zake:
Nimeota ndoto ingine.
Mara hii jua na mwezi
na nyota kumi na moja
zilikuwa zinaniinamia.
Kisha akamuelezea baba yake
ndoto hiyo na pia ndugu zake,
na baba yake akamukemea na kumuambia:
Hii ndoto yako iko na maana gani?
Je, kweli mimi na mama yako pamoja na ndugu zako
tutakuja na kuinama mupaka chini mbele yako?
Na ndugu zake wakaanza kumusikilia wivu,
lakini baba yake akaendelea kuweka
maneno hayo katika akili yake.
Familia ya Yosefu
haipendi kukubali maana ya ndoto zake!
Lakini, Yakobo ‘akaendelea kuweka ile maneno,’
ni kusema, kuweka zile ndoto “katika akili.”
Namna gani?
Anaendelea kufikiri sana juu ya zile ndoto.
Pengine anatambua kama ndoto za
mutoto wake zinatoka kwa Yehova.
Lakini ndugu za Yosefu, wanatenda kwa njia tofauti.
Tusome pamoja Mwanzo 37:18-36.
Sasa wakamuona kwa mbali,
na mbele afike karibu nao,
wakaanza kufanya mupango wa kumuua.
Kwa hiyo wakaambiana:
Angalia! Ule mwota-ndoto anakuja.
Mukuje sasa, tumuue na tumutupe
ndani ya moja ya mashimo ya maji,
na tutasema kwamba munyama
mukali wa pori alimupasua-pasua.
Kisha tuone ndoto zake zitakuwa namna gani.
Wakati Rubeni alisikia maneno hayo,
akajaribu kumuokoa kutoka katika mikono yao.
Kwa hiyo akasema:
Tusiondoe uzima wake.
Rubeni akawaambia:
Musimwange damu.
Mumutupe ndani ya shimo hili la maji
lenye kuwa katika jangwa,
lakini musimuumize.
Alitaka kumuokoa kutoka katika mikono yao
ili amurudishe kwa baba yake.
Kwa hiyo
wakati tu Yosefu alifika mahali ndugu zake walikuwa,
wakamuvua ile kanzu,
ile kanzu ya pekee yenye alikuwa anavaa,
na wakamukamata na kumutupa
ndani ya lile shimo la maji.
Wakati huo lile shimo lilikuwa bila kitu ndani;
halikukuwa na maji.
Kisha wakakaa ili wakule chakula.
Wakati waliinua macho,
kulikuwa musururu wa Waishmaeli
wenye ulikuwa unatoka Gileadi.
Ngamia wao walibeba ubani mweusi, zeri,
na ngozi ya muti yenye utomvu,
na walikuwa wanaenda Misri.
Basi Yuda akaambia ndugu zake:
Tutapata faida gani ikiwa tunamuua
ndugu yetu na kufunika damu yake?
Mukuje sasa, tumuuzishe kwa Waishmaeli,
na tusiweke mukono wetu juu yake.
Kwa vyovyote, yeye ni ndugu yetu na nyama yetu.
Kwa hiyo wakamusikiliza ndugu yao.
Na wakati wale wafanyabiashara
Wamidiani walikuwa wanapita,
wakamutosha Yosefu katika shimo la maji
na wakamuuzisha kwa wale Waishmaeli
kwa vipande makumi mbili vya feza.
Wale wanaume wakamupeleka Yosefu Misri.
Kisha wakati fulani
wakati Rubeni alirudia kwenye lile shimo la maji
na kuona kwamba Yosefu hakukuwa
ndani ya lile shimo la maji,
akapasua nguo zake.
Wakati alirudia mahali ndugu zake
walikuwa, mara moja akasema:
Mutoto haiko!
Na mimi nitafanya nini?
Kwa hiyo
wakakamata kanzu ya Yosefu
na wakachinja mbuzi-dume
na wakatumbukiza-tumbukiza
ile kanzu katika damu hiyo.
Kisha mambo hayo
wakamutumia baba yao ile kanzu ya pekee na kusema:
Hii ndiyo tumepata.
Tafazali chunguza hii uone kama
ni ya mwana wako ao hapana.
Kisha akaichunguza na mara moja akasema:
Ni kanzu ya mwana wangu!
Munyama mukali wa pori anapaswa
kuwa amemupasua-pasua!
Hakika Yosefu amepasuliwa vipande-vipande!
Basi Yakobo akapasua nguo zake na kuvaa
nguo ya gunia kuzunguka kiuno chake
na akamuombolezea mwana wake kwa siku nyingi.
Na watoto wake wote wanaume na
watoto wake wote wanamuke
wakajaribu sana kumufariji,
lakini aliendelea kukataa kufarijiwa, akisema:
Nitashuka ndani ya Kaburi nikiombolezea mwana wangu!
Na baba yake akaendelea kumulilia.
Basi Wamidiani wakamuuzisha Yosefu Misri kwa Potifa,
ofisa wa makao ya Farao na mukubwa wa walinzi.
Mabadiliko makubwa kabisa
alikuwa mutoto mupendwa sana,
sasa ni mutumwa wa hali ya chini!
Ndugu za Yosefu
walikosa upendo mushikamanifu kwa Yosefu,
kwa Yakobo baba yao,
na jambo la maana zaidi, kwa Yehova,
Baba yao wa mbinguni.
Watumishi waaminifu wa Yehova
wanaweza kutendewa bila haki.
Wakati fulani,
muamini mwenzetu anaweza kututendea bila haki.
Unapambana na magumu kama ile?
Kwa kweli,
majaribu inakupatia nafasi ya pekee
ya kuonyesha kama unamupenda Yehova.
Namna gani?
Ona namna Yosefu alitenda wakati alipata majaribu.
Mwanzo 39:1-23 inasema hivi:
Sasa Yosefu akapelekwa Misri.
Na Mumisri mumoja mwenye aliitwa Potifa,
ofisa wa makao ya Farao na mwenye
alikuwa mukubwa wa walinzi,
akamununua kutoka kwa Waishmaeli
wenye walikuwa wamemuleta kule.
Lakini Yehova alikuwa pamoja na Yosefu.
Kwa hiyo
mambo yakamuendea muzuri
na akawekwa juu ya nyumba
ya bwana wake, ule Mumisri.
Na bwana wake akaona kama
Yehova alikuwa pamoja naye
na kama Yehova alikuwa anafanya
kila jambo lenye Yosefu alifanya liendeke muzuri.
Yosefu akaendelea kukubaliwa
mbele ya macho ya bwana wake,
na akakuwa mutumishi wake mwenyewe.
Kwa hiyo Potifa akamuweka juu ya nyumba yake,
na akamuweka asimamie vitu vyake vyote.
Tangu wakati Potifa alimuweka
kuwa musimamizi wa nyumba yake
na wa vitu vyake vyote,
Yehova aliendelea kubariki nyumba
ya ule Mumisri kwa sababu ya Yosefu,
na Yehova akabariki vitu vyote vyenye
Potifa alikuwa navyo katika nyumba
na katika eneo la mashamba.
Mwishowe akaacha kila kitu chenye
kilikuwa chake katika mikono ya Yosefu,
na Potifa hakukuwa anahangaikia kitu kingine
isipokuwa chakula chenye alikuwa anakula.
Tena, Yosefu akakuwa mwanaume
mwenye umbo ya muzuri
na sura ya kupendeza.
Kisha mambo hayo,
bibi ya bwana wake akaanza kumuangalia
na kumutamani sana Yosefu
na kusema:
Lala na mimi.
Lakini akakataa na kumuambia bibi ya bwana wake:
Angalia,
bwana wangu haangaikie kile
ninafanya katika nyumba hii,
na ameweka vitu vyake vyote katika mikono yangu.
Hakuna mwenye kuwa mukubwa
zaidi kuliko mimi katika nyumba hii,
na bwana wangu hakunikataza
kitu chochote isipokuwa wewe,
kwa sababu wewe uko bibi yake.
Kwa hiyo
ninaweza namna gani kufanya ubaya huu mukubwa
na kwa kweli nimutendee Mungu zambi?
Kwa hiyo kila siku alikuwa anasema na Yosefu,
lakini Yosefu hakukubali hata kidogo kulala naye
wala kubakia pamoja naye.
Lakini siku moja wakati Yosefu aliingia
katika nyumba ili kufanya kazi yake,
wafanyakazi wote wa nyumba
hawakukuwa katika nyumba.
Kisha akakamata kwa nguvu nguo ya Yosefu na kusema:
Lala na mimi!
Lakini Yosefu akaacha nguo yake katika
mukono wake na kukimbia inje.
Wakati tu aliona kwamba Yosefu
amemuachia nguo yake na kukimbia inje,
akaanza kuita wanaume wa
nyumba yake na kuwaambia:
Muangalie!
Alituletea mwanaume huyu Mwebrania
ili kutufanya tukuwe kitu cha kuchekwa.
Alikuja ili kulala na mimi,
lakini nilianza kulalamika kwa sauti yangu yote.
Kisha wakati tu alisikia ninasema
kwa sauti kubwa na kulalamika,
akaacha nguo yake pembeni yangu na kukimbia inje.
Kisha mambo hayo
akaweka nguo ya Yosefu pembeni yake
mupaka wakati bwana wake
alirudia katika nyumba yake.
Kisha akamuambia Potifa jambo lilelile, kwa kusema:
Ule mutumishi Mwebrania mwenye ulituletea
alikuja karibu na mimi ili kunifanya
kuwa kitu cha kuchekwa.
Lakini wakati tu nilipandisha sauti na kuanza kulalamika,
aliacha nguo yake pembeni yangu na kukimbia inje.
Wakati tu bwana wa Yosefu alisikia
maneno yenye bibi yake alimuambia, kwa kusema:
“Hayo ndiyo mambo yenye mutumishi wako alinitendea,”
kasirani yake ikawaka.
Kwa hiyo bwana wa Yosefu akamukamata
na kumutia katika gereza,
mahali wafungwa wa mufalme walikuwa wamefungwa,
na Yosefu akabakia kule katika gereza.
Lakini Yehova aliendelea kuwa pamoja na Yosefu
na akaendelea kumuonyesha upendo mushikamanifu
na kumufanya akubaliwe mbele ya
macho ya ofisa mukubwa wa gereza.
Kwa hiyo ofisa mukubwa wa gereza
akamuweka Yosefu kuwa musimamizi
wa wafungwa wote katika gereza,
na kila kitu chenye wafungwa
walikuwa wanafanya ndani ya gereza,
ni yeye alikuwa anaagiza kifanywe.
Ule ofisa mukubwa wa gereza
hakukuwa anaangalia kitu chochote
chenye kilikuwa katika mikono ya Yosefu,
kwa sababu Yehova alikuwa pamoja na Yosefu
na Yehova alifanya kila jambo lenye
Yosefu alifanya liendeke muzuri.
Yehova anaendelea kumuhangaikia Yosefu,
na afanya kila jambo lenye Yosefu
anafanya liendeke muzuri.
Juu ya nini Yehova anamupenda sana Yosefu?
Ni juu Yosefu haache kumupenda Mungu.
Mambo yenye ilimupata Yosefu inatufundisha kama
tukiendelea kumupenda Yehova, hatatuacha!
Lakini, kwa wakati wenye kufaa,
atatutolea kile tuko nacho lazima ili tuweze kuvumilia.
Tukirudia mu habari kumuhusu Yosefu,
tunaona kuwa
anapewa kazi ya kuhangaikia wafungwa wawili wa pekee
mukubwa wa wanyweshaji wa Farao
na mukubwa wa watengenezaji wake wa mikate.
Usiku moja wanaota ndoto zenye kuvuruga.
Yehova anamusaidia Yosefu afasirie
maana ya zile ndoto, na zinatimia.
Katika Mwanzo 40:14,
Yosefu anamuambia mukubwa wa wanyweshaji hivi:
“Unapaswa kunikumbuka wakati
mambo yatakuendea muzuri.
Tafazali unionyeshe upendo mushikamanifu
na unitaje mbele ya Farao, ili nitoke hapa.”
Lakini mukubwa wa wanyweshaji anamusahau Yosefu.
Kisha,
Farao pia anaota ndoto mbili zenye zinamuvuruga
ya kwanza, ngombe wenye kukonda
wanameza wenye kunenepa;
ya pili, masuke ya mubaya inameza ya muzuri.
Makuhani na wanaume wote wenye hekima wa Misri,
wanashindwa kufasiria maana ya zile ndoto.
Mwishowe,
mukubwa wa wanyweshaji anaambia Farao kama
Yosefu iko na uwezo wa ajabu wa kufasiria ndoto.
Yosefu anaitwa haraka.
Turudilie usomaji wetu kuanzia Mwanzo 41:25,
Yosefu, iko sasa na miaka 30, na iko mbele ya mufalme.
Kisha Yosefu akamuambia Farao:
Ndoto za Farao ni moja na ni ileile.
Mungu wa kweli amemuambia
Farao mambo yenye atafanya.
Wale ngombe saba wazuri ni miaka saba.
Pia,
yale masuke saba ya muzuri ya nafaka ni miaka saba.
Ndoto zako ni moja na ni ileile.
Wale ngombe saba wenye kukonda
na wabaya wenye walipanda kisha wale ngombe wazuri
ni miaka saba,
na yale masuke saba ya nafaka yenye hayana kitu,
yenye yalikaushwa na upepo wa mashariki,
itakuwa miaka saba ya njaa.
Ni vile nilimuambia Farao:
Mungu wa kweli amemufanya Farao
aone mambo yenye Atafanya.
“Kutakuwa miaka saba ya chakula
kingi katika inchi yote ya Misri.
Lakini kisha miaka hiyo,
kutatokea miaka saba ya njaa,
na chakula kingi chote chenye
kilikuwa katika inchi ya Misri
hakika kitasahauliwa,
na njaa itaharibu inchi.
Na chakula kingi chenye kilikuwa katika inchi
hakitakumbukwa tena kwa sababu
ya njaa yenye itatokea kisha,
kwa maana itakuwa kali sana.
Ndoto hiyo ilitolewa mara mbili kwa Farao
kwa sababu jambo hilo limefanywa
imara kabisa na Mungu wa kweli,
na Mungu wa kweli atalitimiza hivi karibuni.
Yosefu anaonyesha mufalme
namna ya kupambana na njaa yenye iko inakuja.
Farao anafurahia sana mafasirio ya Yosefu
na shauri lake;
kwa hiyo
anamuweka juu ya inchi yote ya Misri,
anakuwa wa pili kisha tu yeye!
Miaka munane kisha, njaa inapiga kabisa eneo lote.
Familia ya Yosefu inateseka pia na njaa.
Yakobo anatuma watoto wake
waende kuuza chakula Misri.
Watoto kumi wa Yakobo wanaenda Misri.
Lakini Benyamini, ule mudogo zaidi,
anabakia ku nyumba.
Wale ndugu kumi wanakutana na Yosefu na kumuinamia;
wanatimiza ndoto yenye aliota kumepita miaka mingi.
Yosefu anawatambua,
lakini wao hawamutambue.
Anazungumuza nao mu luga ya Wamisri kupitia mutafsiri
na hapendi wamutambue.
Yosefu anapaswa kuamua.
Atatumia mamlaka yake ili kutesa ndugu zake?
Je, atawafukuza, akiwaza kama hapaswe kuwasaidia?
Ao atatafuta nafasi ya kufanya nao amani?
Ataiga upendo mushikamanifu wa Yehova?
Wewe ungefanya nini?
Yosefu anapenda kujua kama
ndugu zake walishabadilika
ao kama wangali wanamuchukia na kumusikilia wivu.
Kwa hiyo,
anawaambia kama ni wapelelezi,
na kama atamufunga Simeoni
mupaka wakati watakuja na Benyamini.
Tusome pamoja Mwanzo 42:21-24.
Hakika
tuko tunapewa azabu kwa sababu ya ndugu yetu,
kwa kuwa tuliona taabu yake wakati
alituomba tumuonyeshe huruma,
lakini hatukusikiliza.
Ndiyo maana musiba huu umetufikia.
Kisha Rubeni akawajibu:
Je, sikuwaambia, ‘Musimutendee mutoto zambi,
lakini hamukukuwa munanisikiliza?
Sasa hakika damu yake iko inaombwa.
Lakini hawakujua kwamba Yosefu alikuwa anaelewa,
kwa sababu kulikuwa mutafsiri katikati yao.
Kwa hiyo akaenda mbali nao na kuanza kulia.
Wakati alirudia na kuzungumuza nao tena,
akamukamata Simeoni kati yao
na kumufunga mbele ya macho yao.
Rubeni
anahuzunika sana juu ya mambo
yenye walimutendea Yosefu.
Rubeni na ndugu zake wametubu kikweli?
Ili kujua,
Yosefu anaomba ndugu zake warudie Kanaani
na wamulete Benyamini,
ule ndugu yao mudogo zaidi.
Yakobo anafanya nini
kisha kusikia kama Benyamini anapaswa kuenda Misri?
Mwanzo 42:36, 37 inajibu hivi:
Ni mimi munafanya nikose watoto!
Yosefu haiko tena,
na Simeoni haiko tena,
na munataka kumukamata Benyamini!
Ni mimi mambo yote hayo yanaangukia!
Lakini Rubeni akamuambia baba yake:
Unaweza kuua wana wangu
wawili kama simulete kwako.
Unipatie yeye, na nitamurudisha kwako.
Yakobo anakataa kabisa!
Hapendi abakie bila Benyamini.
Lakini, katika mwaka wa pili wa ile njaa,
Yakobo na watu wa nyumba yake hawana tena chakula.
Yakobo atakubali Benyamini
aende na ndugu zake kule Misri
ili walete chakula ingine?
Tuone jibu mu andiko la Mwanzo 43:8-10, 13, 14.
Kisha Yuda akamulilia Israeli baba yake:
Tuma kijana huyu pamoja na mimi,
na utuache tuende ili tuweze kuishi na tusikufe
sisi na wewe na watoto wetu.
Nitahakikisha iko salama.
Utamuomba katika mikono yangu.
Kama simurudishe kwako na kumuleta kwako,
nitakuwa nimekutendea zambi kwa wakati wote.
Lakini kama hatungekuwa tumekawia,
kufikia sasa tungekuwa tumefika
kule na kurudia mara mbili.
Mumuchukue ndugu yenu na muende,
murudie kwa ule mwanaume.
Mungu Mweza-Yote
amuchochee mwanaume huyo awaonyeshe huruma,
ili amuachilie
na kuwapatia ule ndugu yenu mwingine na Benyamini.
Lakini kwa upande wangu,
kama ni lazima nikose watoto, nitakosa watoto!
Hata kama zamani Yuda hakusikilia huruma Yosefu
mutoto mupendwa sana wa baba yake,
sasa, iko tayari kulinda Benyamini,
mutoto mupendwa sana wa baba yake.
Kwa hiyo, Yakobo anakubali watoto wake warudie Misri,
na wanamupelekea Yosefu zawadi.
Tuendelee basi na usomaji wetu
katika Mwanzo 43:26-30.
Wakati Yosefu aliingia katika nyumba,
wakamupelekea zawadi yao
na wakainamisha uso mupaka chini mbele yake.
Baba yenu ule muzee mwenye mulisema juu yake
iko namna gani?
Angali muzima?
Basi wakasema:
Mutumishi wako baba yetu iko muzuri.
Angali muzima.
Kisha wakainama na kushusha uso chini.
Wakati aliinua macho na kumuona
Benyamini ndugu yake,
mwana wa mama yake, akasema:
Je, huyu ndiye ndugu yenu mudogo zaidi
mwenye muliniambia juu yake?
Akaongeza kusema:
Mungu akuonyeshe wema, mwana wangu.
Halafu Yosefu akafanya haraka,
kwa maana alilemewa na hisia
kwa sababu ya ndugu yake,
na akatafuta mahali pa kulilia.
Kwa hiyo
akaingia katika chumba chenye hakikukuwa na watu
na akaanza kutoa machozi kule.
Yosefu anapenda kujua kama
ndugu zake wamebadilika kabisa,
kwa hiyo anawajaribu.
Namna gani?
Yosefu anaomba watumishi wake
wajaze chakula mu mifuko ya ndugu zake.
Kwa siri,
anawaomba watie kikombe chake cha
feza mu mufuko wa Benyamini.
Kisha wote kuondoka na kufika mbali kidogo,
Yosefu anatuma watumishi wake wawafuate.
Kisha kuwakuta, wanawauliza:
‘Juu ya nini mumeiba kikombe
cha feza cha bwana wetu?’
Ndugu za Yosefu wanakataa kabisa, na wanasema:
‘Ikiwa kinapatikana kwa mumoja kati yetu,
ule mutu auawe.’
Wale watumishi wanatafuta mu mifuko yote,
na wanapata kile kikombe mu mufuko wa Benyamini!
Ndugu zake wanaonyesha huzuni
yao kwa kupasua nguo zao.
Hawajue wafanye nini,
kwa hiyo wanarudia na Benyamini kwa Yosefu.
Kisha kuanguka chini mbele ya Yosefu,
Yuda anasema:
“Mungu wa kweli amefunua kosa la watumwa wako.
Sasa sisi tuko watumwa wa bwana wangu.”
Lakini, Yosefu,
anaendelea kuwajaribu, na anawaambia hivi waziwazi:
‘Ninyi wengine murudie,
lakini Benyamini atabakia hapa akuwe mutumwa wangu!’
Yuda anamulilia hivi:
‘Kama simurudishe Benyamini,
hakika baba yangu atakufa
na nitakuwa nimetutendea zambi milele.’
Yuda hapendi baba yake ateseke juu ya kukosa
mutoto mwingine mwenye anapenda sana;
anajitolea akuwe mutumwa pa nafasi ya Benyamini.
Tuone vile Yosefu anatenda katika Mwanzo 45:1-15:
Wakati huo
Yosefu hakuweza tena kujizuia
mbele ya watumishi wake wote.
Kwa hiyo akasema kwa sauti kubwa:
Mutoshe kila mutu mbele yangu!
Hakuna mutu mwingine mwenye alibakia pamoja naye
wakati Yosefu alijitambulisha
mwenyewe kwa ndugu zake.
Kisha akaanza kulia kwa sauti kubwa
mupaka Wamisri wakasikia
na nyumba ya Farao ikasikia.
Mwishowe Yosefu akaambia ndugu zake:
Mimi ni Yosefu.
Je, baba yangu angali muzima?
Lakini ndugu zake hawakuweza kumujibu,
kwa maana walishituka sana kwa sababu yake.
Kwa hiyo Yosefu akaambia ndugu zake:
Tafazali, munikaribie.
Basi wakamukaribia. Kisha akasema:
Mimi ni Yosefu ndugu yenu,
mwenye muliuzisha apelekwe Misri.
Lakini sasa musihuzunike
na kila mumoja asimulaumu mwenzake
kwa sababu muliniuzisha huku;
kwa sababu Mungu alinituma mbele yenu
ili kulinda uzima.
Huu ni mwaka wa pili wa njaa katika inchi,
na kungali miaka tano yenye
hakutakuwa kulima wala kuvuna.
Lakini Mungu alinituma mbele yenu
ili kulinda mabaki kwa ajili yenu juu ya dunia
na kuwaokoa kwa wokovu mukubwa.
Kwa hiyo basi,
haiko ninyi ndio mulinituma huku,
lakini ni Mungu wa kweli,
ili aniweke kuwa mushauri mukubwa wa Farao
na bwana kwa ajili ya nyumba yake yote
na mutawala juu ya inchi yote ya Misri.
“Murudie haraka kwa baba yangu,
na munapaswa kumuambia,
‘Mwana wako Yosefu anasema:
“Mungu ameniweka kuwa bwana juu ya Misri yote.
Shuka ukuje kwangu.
Usikawie.
Unapaswa kukaa katika inchi ya Gosheni,
mahali kwenye utakuwa karibu na mimi
wewe, wana wako, wajukuu wako, makundi yako,
mifugo yako, na kila kitu chenye uko nacho.
Nitakupatia chakula kule,
kwa maana kungali miaka tano ya njaa.
Kama haiko vile, utakuwa maskini,
wewe na nyumba yako na kila kitu chenye uko nacho.’”
Ninyi na ndugu yangu Benyamini
munajionea na macho yenu wenyewe
kwamba ni mimi ninazungumuza na ninyi.
Kwa hiyo munapaswa kumuambia baba yangu
kuhusu utukufu wangu katika Misri
na kila kitu chenye mumeona.
Sasa mufanye haraka na mumulete baba yangu hapa.
Kisha akamukumbatia Benyamini
ndugu yake na akaanza kulia,
na Benyamini akalia na mikono ya
Yosefu ilikuwa imezunguka shingo ya Benyamini.
Na akabusu ndugu zake wote
na akalia juu ya shingo zao.
Kwa hiyo,
Yakobo, pamoja na watu karibu 70 wa familia yake,
wanashuka kuenda Misri.
Farao anawapatia inchi ya Gosheni ili waishi mule.
Kwa miaka 215,
wazao wa Yakobo wanakaa mu inchi ya Misri
mupaka siku yenye wote milioni tatu ao zaidi
wanavuka Bahari Nyekundu,
na kisha wanaingia mu Inchi ya Ahadi.
Yehova alitumia Yosefu ili kulinda
kizazi mwenye Masiya angetokea.
Hadisi kumuhusu Yosefu inatufundisha nini?
Hata kama alipambana na hali gani,
Yosefu alimuonyesha Yehova upendo mushikamanifu.
Kwa miaka mingi alipata magumu yenye ilifuatana,
lakini hakuweka kinyongo hata kidogo.
Leo, mara mingi ni nguvu kuzuia majaribu yenye inaweza kutupata katika huu ulimwengu.
Lakini tunaweza kuamua namna ya kupambana nayo.
Tunaepuka kumukasirikia Yehova.
Tunamupenda Yehova,
na tumeazimia kumuonyesha upendo
kwa kuepuka mwenendo wowote
wenye unaweza kumuumiza.
Kisha, wakati hali ya Yosefu ilibadilika,
alionyesha familia yake upendo mushikamanifu,
hata kama ndugu zake walimutendea mubaya.
Kwa kweli, upendo mushikamanifu wa Yosefu
kwa familia yake,
ulisaidia kutimiza unabii!
Mu siku za Abrahamu,
babu ya baba wa Yosefu,
Yehova aliweka wakati wa kukomboa watu wake
miaka 430 kisha.
Kama Yosefu hakuonyesha familia
yake upendo mushikamanifu,
namna gani ule unabii ungetimia?
Ni wazi kuwa,
kuonyesha ndugu zetu upendo mushikamanifu,
ni jambo la maana mbele ya Yehova.
Kwa hiyo kama umeumizwa na ndugu yako wa kiroho,
usiangukie mu mutego wa kumusema
mubaya mbele ya watu
ao kumuumiza.
Ujikaze kurudisha amani.
Zaidi ya ile,
ndugu zetu wanapendwa na Yehova.
Wanastahili tuwaonyeshe upendo!
Katika hii habari,
Yehova ni mufano muzuri zaidi katika
kuonyesha upendo mushikamanifu.
Yosefu alikataliwa na familia yake,
alisemewa uongo na bibi ya mukubwa wake wa kazi,
na kisha alifungwa;
lakini Yehova “aliendelea kuwa pamoja na Yosefu
na akaendelea kumuonyesha upendo mushikamanifu.”
Juu ya nini?
Ni juu alibakia mushikamanifu,
kwa hiyo alimutendea kwa ushikamanifu.
Yehova alionyesha pia
upendo mushikamanifu kwa taifa lote la Israeli
kupitia namna alimutendea Yosefu.
Kwa kumutumia ili kulinda familia yake,
Yehova alilinda kizazi mwenye Masiya angetokea
na alihakikisha kuwa ahadi yake ya kukomboa Waisraeli
inatimia kwa wakati.
Ile inatutia moyo sana.
Wanadamu wenye hawakamilike
wanaweza kukuvunja moyo,
kukuzarau, kukusemea uongo, ao kukutendea bila haki.
Lakini ukibakia muamifu, Yehova hawezi kukuacha.
Hakumusahau Yosefu hata kidogo,
na hatasahau hata mumoja wa
watumishi wake waaminifu.
Bakia karibu na Yehova,
na ataendelea kukuonyesha upendo mushikamanifu.