JW subtitle extractor

Ufalme wa Mungu Ulianza Kutawala Mwaka wa 1914

Video Other languages Share text Share link Show times

Tangu wanadamu wa kwanza
walipomkataa Yehova
Mungu kuwa Mtawala
ulimwengu wetu umejaa
uovu na kuteseka.
Lakini Yesu alitupatia tumaini.
Alifundisha kwamba akiwa
Mfalme wa Ufalme wa Mungu,
atarudisha amani na haki duniani.
Ufalme huo ungeanza
kutawala lini?
Kulingana na Biblia,
tayari Ufalme huo
umeanza kutawala.
Tunajuaje?
Fikiria jambo lililotekea
zaidi ya miaka 2,600 iliyopita.
Yehova Mungu
alimfanya Nebukadneza
Mfalme wa Babiloni la kale
aote ndoto ya kinabii.
Katika ndoto hiyo,
Nebkadneza aliona
mti mrefu sana uliofika mbinguni.
Mti huo ulikatwa,
lakini kisiki chake kikabaki ardhini.
Baada ya kipindi cha “nyakati saba”
mti huo ulikua tena.
Biblia inaonyesha kwamba
ndoto hiyo ingetimizwa kwa njia mbili.
Kwanza ingetimizwa
kuhusiana na Mfalme Nebukadneza.
Alikuwa mashuhuri
na mwenye nguvu sana.
kama mti huo mrefu uliofika mbinguni.
lakini alikatwa kwa “nyakati saba.”
Hilo lilitokea wakati Nebukadneza
alipokuwa wazimu kwa miaka 7.
Katika kipindi hicho
hangeweza kutawala akiwa Mfalme.
Baada ya nyakati hizo saba
Nebukadneza alirudiwa na akili
akaanza kutawala tena.
Huo ulikuwa utimizo wa
kwanza wa unabii huu.
Unabii huo ulitimizwaje
kwa njia ya pili?
Ni kuhusiana na utawala wa Mungu.
Biblia inasema,
Wafalme katika Israeli ya kale,
waliketi kwenye kiti
cha Ufalme cha Yehova.
Yaani, walimwakilisha Mungu
na utawala wake.
Lakini wengi wa wafalme hao
walikosa kumtii Yehova
na pia wengi kati ya
raia wao hawakumtii.
Kwa sababu ya kutotii
Mungu aliruhusu Waisraeli
washindwe na Wababiloni
ambao waliharibu jiji la Yerusalemu
mwaka wa 607 K.W.K.
Tangu wakati huo,
hakuna wafalme waliomwakilisha
Yehova huko Yerusalemu.
Basi 607 K.W.K
ulikuwa mwanzo
wa zile “nyakati saba”
au kipindi ambacho
utawala wa Mungu ungekatizwa.
Kipindi hicho kingeendelea
mpaka Yehova
amweke Mfalme mpya
ambaye angemwakilisha,
Mfalme aliye mbinguni.
Hilo lingetokea lini?
Katika utimizo wa pili wa unabii huo
zile nyakati saba
zingekuwa kipindi kirefu
kuliko miaka 7.
Tunajuaje?
Kwanza, miaka 7 baada ya
Yerusalemu kuharibiwa
hakuna jambo muhimu lililotokea
kuhusiana na utawala wa Mungu.
Na karne nyingi baadaye,
Yesu alionyesha
kwamba zile “nyakati saba”
hazikuwa zimeisha.
Katika unabii kuhusu siku za mwisho
Yesu alisema kwamba
utawala wa Mungu au Yerusalemu
“litakanyagwakanyagwa na mataifa
mpaka nyakati zilizowekwa
za mataifa zitimie.”
“Nyakati zilizowekwa za mataifa”
ni sawa na zile “nyakati saba.”
Nyakati hizo zingekwisha lini?
Kitabu cha Biblia cha
Ufunuo kinasema kwamba
“nyakati tatu na nusu”
ni sawa na siku 1,260.
Basi nyakati saba
ni mara mbili ya idadi hiyo
au siku 2,520.
Katika unabii wa Biblia, siku moja
inaweza kuwakilisha mwaka mmoja.
Ndivyo ilivyo kuhusu
ule unabii wa “nyakati saba”
zinawakilisha miaka 2,520.
Tukianzia mwaka wa 607 K.W.K
miaka 2,520
inatufikisha kwenye mwaka wa 1914
mwaka ambao zile
“nyakati saba” zilikwisha
na Yesu akaanza kutawala mbinguni
akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu.
Huo ulikuwa mwanzo wa
kipindi ambacho Biblia inakiita
“siku za mwisho.”
Hivi karibuni,
Yesu atamaliza kazi ya
kuwakusanya watawala wenzake
wajiunge naye mbinguni.
Kisha, Ufalme wa Mungu
utaondoa matatizo yote
yanayotupata sisi na familia zetu.
Wazia ukiishi wakati huo
chini ya utawala wa Mfalme
ambaye anakujali sana.