JW subtitle extractor

Shangilia Katika Ahadi za Mungu za Amani—Kisehemu

Video Other languages Share text Share link Show times

Je, unatamani kuwa na nyumba yako mwenyewe?
Yehova aliwaahidi wahamishwa waliokuwa wakirudi,
kwamba wangejenga
na kufurahia makao yenye kustarehesha.
Vivyo hivyo,
Yehova anatujali pia.
Iwe tunapoteza makao yetu,
au tunafukuzwa kutoka huko.
Zaidi ya yote,
ibada ya kweli
inatuandalia usalama wa kiroho
ambao hauwezi kupatikana mahali popote.
Makao ya kiroho tunayofurahia leo,
yanatukumbusha kwamba
Yehova atatupatia makao halisi
katika ulimwengu mpya.
“Watajenga nyumba
na kuishi ndani yake.”
Ikiwa ungekuwa unafunga safari ndefu
ungehisije ikiwa ungejua kwamba,
utakutana na wahalifu
au wanyama hatari?
Yehova aliwahakikishia wahamishwa waliokuwa wakirudi,
kwamba wangesafiri kwa usalama
na kuishi kwa amani.
Katika paradiso ya kiroho
tunayofurahia sasa hivi,
watu ambao wakati fulani walikuwa wenye jeuri,
wamejifunza kuwa wanyenyekevu,
wenye upendo
na wenye kufanya amani.
Wazia amani itakayokuwepo katika ulimwengu mpya wa Mungu,
wakati ambapo tutaweza kutembea
katika sayari hii maridadi,
tuchunguze kila kona
na kufurahia kazi ya Mungu wa kweli,
bila woga.
“Hawatadhuru
wala kusababisha uharibifu wowote
katika mlima wangu wote mtakatifu,
asema Yehova.”
Kupata maagizo ya wazi
kutoka kwa Yehova,
hutusaidia tumkaribie.
Na kunatusaidia
kudumisha afya ya kiroho.
Mafundisho ya Uwongo yanapozidi kuwafunga watu katika giza la kiroho,
Yehova anatuandalia uhuru wa kweli.
Afya ya kiroho tunayofurahia leo,
inatukumbusha kwamba
afya kamilifu ya kimwili na kiakili,
itakuwepo katika paradiso.
Wazia ukiamka kila siku,
ukijihisi ukiwa safi,
ukiwa na afya nzuri,
ukiwa na furaha,
na ukiwa na shangwe kamili maishani,
Yehova anaahidi:
“Hakuna mkaajia atakayesema
mimi ni mgonjwa.”
Yehova alitimiza ahadi aliyowapa wahamishwa,
aliirudisha nchi hiyo iliyokuwa magofu,
kana kwamba anairudisha kuwa hai.
Mwaka wa 1919,
Yehova alifanya jambo kama hilo.
Aliwaweka huru watu wake
kutoka kwenye utekwa wa kiroho,
kisha akawachochea waanze kuhubiri.
Kama tu Yehova alivyowainua watu wake
kutoka katika kifo cha mfano,
atafanya vivyo hivyo kuhusiana na kifo halisi.
Kwa kweli
Mungu atameza kifo,
milele.
Wazia ukiishi muda mrefu kuliko mti wowote,
kwa sababu
kifo hakitakuwapo tena.