JW subtitle extractor

Utangulizi wa Mwanzo

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa kitabu cha Mwanzo.
Musa alikamilisha uandikaji wa
kitabu cha Mwanzo
katika nyika ya Sinai
mwaka wa 1513 K.W.K.
Musa alizaliwa mwaka wa 1593 K.W.K.,
na alikuwa nabii,
kiongozi,
mwamuzi,
mwanahistoria, na mpatanishi.
Aliandika vitabu vitano vya
kwanza vya Biblia
vinavyoitwa Pentateuki,
kutia ndani vitabu vya Ayubu,
Zaburi 90, na labda pia Zaburi 91
Neno Mwanzo
linamaanisha “chimbuko,” au “asili.”
Kitabu hicho kinaeleza
jinsi ulimwengu ulivyoanza
na jinsi Mungu alivyoitayarisha dunia
ili watu waishi ndani yake.
Pia, simulizi hilo
linafafanua chanzo cha Waisraeli
na jinsi taifa hilo lilivyoongezeka
nchini Misri
hadi kifo cha Yosefu mnamo
1657 K.W.K.
Mwanzo ina sura 50.
Sura ya 1 na ya 2
inaonyesha jinsi Mungu
alivyoandaa dunia
kwa ajili ya wanadamu
kwa vipindi sita vinavyoitwa siku,
na kuumba mwanamume na
mwanamke wa
kwanza, Adamu na Hawa.
Walipaswa ‘kuijaza dunia
na kuitiisha,’
na wangeweza kuishi milele.
Katika sura ya 3,
Hawa alishawishiwa na nyoka
kumwasi Mungu.
Adamu alijiunga naye katika uasi huo,
na hilo linafanya wanadamu wote
warithi dhambi na kifo.
Katika sura ya 6,
malaika waovu
wanavaa miili ya kibinadamu
na kuchukua wanawake
wawe wake zao,
na kutokeza majitu yaliyoitwa Wanefili.
Dunia ikajaa uovu,
na Mungu akaamua
“kuwaangamiza wanadamu wote”
kupitia gharika kubwa.
Hata hivyo,
Noa alipata kibali cha Mungu,
kwa hiyo, Mungu
akamwambia ajenge safina
ili kuokoa familia yake
na aina mbalimbali za wanyama.
Katika sura ya 10 na 11,
tunasoma kwamba baada ya Gharika,
watu walianza kujenga jiji
na mnara mrefu,
na hivyo kupinga kusudi la Mungu
la wanadamu kuijaza dunia.
Lakini Mungu
akavuruga lugha yao na hivyo
kuwatawanya duniani pote.
Sura ya 11 hadi 25
zinaeleza kumhusu Abrahamu
mwanamume mwenye imani.
Katika sura ya 12,
Yehova anamwambia Abrahamu
ambaye wakati huo aliitwa Abramu
aingie katika nchi ambamo
siku moja atakuwa taifa kubwa
na kupitia kwake watu wa
mataifa yote watabarikiwa.
Katika sura ya 15,
Yehova anamwambia
aangalie juu na kuhesabu nyota
ikiwa anaweza.
Mungu akamwambia:
“Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.”
Je, ulijua?
Kitabu cha Mwanzo
kinaonyesha wazi
kichwa kikuu cha Biblia yote:
kutetewa kwa haki ya
Yehova ya kutawala
na kutimizwa kwa kusudi lake
kuelekea dunia na wanadamu
kupitia Ufalme wake
utakaotawaliwa na
mtu ambaye angezaliwa wakati ujao.
Mzao huyo
alitabiriwa kwa mara ya kwanza
kwenye Mwanzo 3:15
pamoja na mambo ambayo angetimiza.
Kitabu cha Ufunuo
kinaonyesha jinsi mzao huyo
atakavyomponda “nyoka wa zamani,”
Shetani,
na kuwaletea wanadamu
wote watiifu baraka zilizoahidiwa.
Katika sura ya 19,
Mungu anaangamiza
Sodoma na Gomora
na majiji ya karibu kwa sababu ya
upotovu wao wa maadili.
Katika sura ya 22,
Yehova anamwambia Abrahamu
amtoe mwana wake Isaka
kuwa dhabihu.
Lakini Abrahamu
alipokuwa akifanya hivyo,
Yehova akamzuia
na kumhakikishia ahadi yake
kuhusu uzao wake wa wakati ujao.
Sura ya 24 hadi ya 50
zinazungumzia hasa kuhusu Isaka,
Yakobo na Esau,
na Yosefu, mwana wa Yakobo.
Isaka anambariki Yakobo,
ambaye anasafiri kwenda Padan-aramu.
Akiwa huko, Yakobo
anapata watoto wengi, kutia ndani
wana 11,
kupitia Lea,
Raheli,
na vijakazi wao wawili.
Kisha Yakobo
akarudi Kanaani,
ambako Mungu alibadili jina lake
na kumwita Israeli.
Akiwa huko Raheli akazaa
mwana wa mwisho wa Yakobo.
Sura ya 37 hadi 41
zinaonyesha jinsi Yosefu,
akiwa na umri wa miaka 17
aliuzwa na ndugu zake
akawa mtumwa wa Potifa,
ofisa wa makao ya Farao.
Mke wa Potifa
alijaribu kumshawishi Yosefu
lakini akashindwa.
Akamsingizia kwamba
alitaka kumbaka,
kwa hiyo, Yosefu
akafungwa gerezani.
Alipokuwa na umri wa miaka 30
huku bado akiwa mfungwa,
kwa msaada wa roho ya Mungu,
Yosefu alitafsiri ndoto za Farao.
Kwa sababu hiyo,
Yosefu akawekwa huru na
kuwa ofisa mkuu wa nchi ya Misri.
Katika sura ya 42 hadi 47,
Yosefu anaunganishwa tena
na familia yake,
ambao wanahamia nchini Misri na
kuwa wakaaji wageni.
Sura ya 49
inaonyesha unabii ambao
Yakobo alitoa kuhusu
watoto wake alipokuwa akifa.
Ukoo wa Yuda
utatokeza uzao ulioahidiwa,
yaani, Shilo,
ambaye “mataifa yatamtii.”
Unaposoma kitabu cha Mwanzo,
ona jinsi kinavyoeleza chanzo cha
kuteseka kwa wanadamu,
uone jinsi wazee wa ukoo
walivyopata kibali na baraka za Mungu,
na jinsi ahadi ambazo
Yehova aliwapa wanaume
hao wenye imani
zinavyoelekeza kwa Yesu Kristo,
Mfalme wa Ufalme wa Mungu.