JW subtitle extractor

Utangulizi wa Kutoka

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa Kitabu cha Kutoka
Kitabu cha Kutoka kiliandikwa na Musa
kwenye jangwa la Sinai
katika mwaka wa 1512 K.W.K.
mwaka mmoja
baada ya Waisraeli kutoka Misri.
Kitabu hicho kinazungumzia miaka 145,
kuanzia kifo cha Yosefu
mwaka wa 1657 K.W.K.
hadi kwenye ujenzi wa hema la ibada
mwaka wa 1512 K.W.K.
Kinasimulia jinsi Yehova alivyowakomboa
Waisraeli kutoka utekwani Misri,
jinsi alivyowapanga wakiwa taifa,
na jinsi alivyowafundisha kumwabudu.
Kitabu cha Kutoka kina sura 40.
Katika sura ya 1,
tunajifunza kwamba
Waisraeli waliongezeka sana,
hivi kwamba Farao
aliwatumikisha kwa ukatili.
Sura ya 2 hadi ya 4 inasimulia
kuhusu kuzaliwa kwa Musa,
jinsi alivyolelewa na binti ya Farao,
na jinsi alivyokimbilia Midiani baada ya
kumuua Mmisri
aliyekuwa akimdhulumu Mwebrania.
Miaka mingi baadaye,
Yehova alimpa Musa
utume wa kuwaongoza
Waisraeli kutoka Misri.
Katika sura ya 7 hadi 10,
kupitia kwa Haruni ndugu yake,
Musa anamwambia Farao tena na tena
awaruhusu Waisraeli waondoke,
lakini Farao anakataa.
Kwa sababu hiyo,
Yehova analeta mapigo
kumi dhidi ya Misri.
Mapigo hayo yanatia ndani
kugeuza Mto Nile kuwa damu,
nchi kujaa vyura,
na wanadamu na wanyama
kupigwa kwa majipu.
Katika sura ya 12,
Mungu anaanzisha Pasaka.
Pia analeta pigo la kumi,
la mwisho,
kuuawa kwa wazaliwa wa kwanza.
Hatimaye, Farao akiwa ameaibishwa,
na mwana wake akiwa
kati ya wale waliokufa,
anawaambia Waisraeli waondoke.
Katika sura ya 13,
akitumia nguzo ya wingu mchana
na nguzo ya moto usiku.
Yehova anawatangulia watu wake
akiwaweka huru kutoka Misri.
Katika sura ya 14 na ya 15,
kwa upumbavu
Farao anawafuata Waisraeli,
lakini Yehova anamzamisha
katika Bahari Nyekundu
pamoja na jeshi lake lote.
Musa na Waisraeli wanamwimbia
Yehova wimbo wa ushindi.
Je, ulijua?
Kupitia Musa,
Yehova alimwambia Farao hivi:
“Nimekuacha uendelee
kuishi kwa sababu hii hasa:
ili nikuonyeshe nguvu zangu
na ili jina langu
litangazwe katika dunia yote.”
Na kwa kweli,
jina la Mungu lilijulikana sana.
Hata hivyo, miaka 40 baadaye,
watu wa Kanaani,
kutia ndani Rahabu kule Yeriko,
walikumbuka matukio ya
Bahari Nyekundu.
Jambo muhimu hata zaidi,
kifo cha aibu cha Farao kinatoa onyo
kwa wote wanaompinga Yehova,
kutia ndani Shetani.
Katika sura ya 16,
Yehova anawaandalia Waisraeli mana,
nacho kinakuwa chakula chao kikuu
muda wote wa safari yao jangwani.
Katika sura ya 19,
Musa anapanda juu ya Mlima Sinai,
ambapo Mungu anaahidi
ikiwa Waisraeli watamtii kabisa,
watakuwa kwake
“ufalme wa makuhani na taifa takatifu.”
Katika sura ya 20,
watu wanashuhudia ngurumo na radi,
sauti ya pembe,
na Mlima Sinai ukifuka moshi
wakati ambapo Mungu
alitoa zile Amri Kumi.
Katika sura ya 24,
Musa anawasomea watu
kitabu cha agano.
Nao wanasema:
“Mambo yote ambayo
Yehova amesema
tuko tayari kuyafanya.”
Sura ya 25 hadi ya 40
zinazungumzia hasa ukuhani,
ujenzi wa hema la ibada,
sanduku la agano,
kinara cha taa,
na vyombo vingine vitakatifu.
Sura ya 28 na ya 29
inakazia hasa mavazi ya makuhani
na kuwekwa rasmi kwa makuhani.
Mavazi ya kuhani mkuu yanatia ndani efodi
na kilemba kilicho na bamba la dhahabu.
Bamba hilo lilikuwa na maneno haya
“Utakatifu ni wa Yehova.”
Katika sura ya 32,
Musa alipokuwa bado juu ya Mlima Sinai,
watu walitengeneza ndama wa dhahabu
na wakaiabudu na
kucheza dansi na kuimba.
Musa aliporudi,
aliiteketeza na kuipondaponda,
na akanyunyiza ungaunga wake juu ya maji
na kuwalazimisha Waisraeli wayanywe.
Katika sura ya 34,
Musa,
akiwa tena juu ya Mlima Sinai,
anamsikia Yehova akitangaza jina lake
na sifa zake.
Sura ya 40 inatueleza
kwamba nguzo ya wingu ilifunika
hema la ibada lililokamilishwa,
na hivyo kulijaza utukufu wa Mungu.
Unaposoma kitabu cha Kutoka,
ona jinsi Yehova anavyowaaibisha
wenye kiburi na wakaidi,
jinsi anavyowatumia
wanyenyekevu na wapole,
na jinsi ukombozi wa Waisraeli
unavyoimarisha imani yetu
katika ukombozi wetu wa wakati ujao
kupitia Ufalme wa Mungu.