JW subtitle extractor

Utangulizi wa Mambo ya Walawi

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa kitabu cha Mambo ya Walawi.
Kitabu cha Mambo ya Walawi
kiliandikwa na Musa
katika mwaka wa 1512 K.W.K.,
katika nyika ya Sinai
kilipewa jina hilo baadaye,
jina hilo linatokana na neno la
Kigiriki linalomaanisha
“Yanayowahusu Walawi.”
Hata hivyo, kitabu hicho
hakikuandikwa kwa ajili Walawi pekee
bali kwa ajili ya taifa lote la Israeli.
Kitabu cha Mambo ya Walawi
kinazungumzia mambo yaliyotokea
ndani ya mwezi mmoja,
na kinasimulia mambo yaliyotokea
mara baada ya ujenzi wa hema la ibada.
Kitabu cha Mambo ya Walawi
kinakazia utakatifu wa Yehova
na kwamba watu wa Yehova wanaweza
kuwa watakatifu kwa kutii amri zake.
Sura ya 1 hadi ya 7
zinataja sheria mbalimbali
kuhusu dhabihu
zinazopaswa kutolewa kwa Yehova.
Sura ya 8 na 9
zinazungumzia mambo yanayohusiana
na kuwekwa rasmi kwa ukuhani,
kutiwa mafuta kwa Haruni
kuwa Kuhani Mkuu,
na dhabihu za kwanza
ambazo Haruni alimtolea Mungu.
Katika sura ya 10,
Yehova anawaua wana wawili wa Haruni,
Nadabu na abihu waliokuwa makuhani
kwa sababu ya kutoa “moto haramu”
au kufukiza uvumba.
Kisha Yehova anatoa amri
kwamba makuhani hawapaswi kunywa kileo
kabla ya kuingia katika hema la mkutano
au hema la ibada.
Sura ya 11 hadi ya 15
zinaonyesha sheria kuhusu
vitu safi na visivyo safi.
Kuhusu chakula,
Yehova anawaambia Waisraeli
ni viumbe gani wanavyoweza kula
na vipi hawawezi kula.
Sura ya 16 inatoa maagizo
kuhusu Siku ya Kufunika dhambi.
Sura ya 17 hadi 20
inaonyesha sheria
kuhusu mwenendo mtakatifu.
Kwa mfano, watu wa Mungu
hawapaswi kula damu,
kujihusisha katika aina yoyote ya
ibada ya sanamu,
au kuwasiliana na pepo
kama mataifa yaliyowazunguka yalivyofanya.
Wanapaswa kuwaonyesha ufikirio
vipofu,
viziwi
na wageni.
Na wanapaswa kuwaheshimu waliozeeka.
Je, ulijua?
Mipango inayotajwa katika
kitabu cha Mambo ya Walawi
ilikuwa “kivuli cha mambo
mema yatakayokuja,”
kama inavyoelezwa
katika kitabu cha Waebrania.
Kwa mfano,
kuhani mkuu anawakilisha Yesu Kristo,
damu ya dhabihu za wanyama
iliwakilisha damu ya Yesu,
Patakatifu Zaidi pa hema la ibada
paliwakilisha “mbinguni kwenyewe”
ambako Yesu aliingia
“mbele za Mungu kwa ajili yetu.”
Sura ya 21 na 22
inaonyesha sheria za kutumikia kama kuhani.
Kwa mfano,
kuhani hakupaswa kuwa na ulemavu wowote
yaani hakupaswa kuwa na
kasoro yoyote mwilini mwake.
Sura ya 23 na 24
ina maagizo kuhusu sherehe na siku takatifu.
Pia, Yehova anatoa mwongozo
kuhusu taa katika hema la ibada
na kuhusu mikate ya wonyesho ya mviringo.
Sura ya 24 inakazia pia
utakatifu wa jina la Mungu.
Kwa amri ya Yehova,
mtu aliyetukana jina la Mungu
alipigwa kwa mawe.
Sura ya 25 ilikuwa na sheria
kuhusu mwaka wa Sabato,
mwaka wa mwadhimisho wa miaka 50,
kurudishwa kwa mali
na jinsi ya kuwatendea maskini.
Wale waliouzwa utumwani
walipaswa kutendewa kwa fadhili
kama wanaofanya kazi ya kibarua.
Sura ya 26 inaonyesha
baraka za kuwa mtiifu kwa Yehova
na adhabu ya kukosa kutii.
Sura ya 27 inamalizia
kitabu cha Mambo ya Walawi
kwa kuonyesha sheria
kuhusu vitu vilivyowekwa nadhiri kwa Yehova
na vitu vilivyotolewa kwake.
Unaposoma kitabu cha Mambo ya Walawi,
ona jinsi tunavyopaswa kujitahidi
kuwa watakatifu kwa kumwiga Yehova;
kwa nini tunapaswa
kuliheshimu sana jina lake takatifu;
na kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kamili
kwamba dunia yote
itaonyesha utakatifu wa Mungu
wakati wa utawala wa Mwana wake,
yule Kuhani Mkuu
na Mfalme wa Ufalme wa Mungu.