JW subtitle extractor

Utangulizi wa Hesabu

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa kitabu cha Hesabu.
Kitabu cha Hesabu kiliandikwa na Musa.
Alianza kukiandika
alipokuwa kwenye nyika ya Sinai
na kukikamilisha katika
jangwa tambarare la Moabu.
Kinasimulia mambo yaliyotukia katika
kipindi cha miaka 38 na miezi 9,
kuanzia 1512 hadi 1473 K.W.K.
Musa alipokamilisha uandikaji wake.
Jina Hesabu linatokana na
mara mbili ambazo Musa aliwahesabu watu.
Kwanza kwenye Mlima Sinai,
halafu baadaye kwenye
jangwa tambarare la Moabu.
Kitabu hicho kinakazia uwezo wa Yehova
wa kuwaongoza watu wake,
kinakazia uhitaji wa kuwatii wanaume
waliowekwa rasmi na Mungu
ili kumwakilisha,
na kinaonyesha umuhimu wa
kuwa na imani yenye nguvu.
Kitabu cha Hesabu kina sura 36.
Katika sura ya 1 hadi ya 4,
Waisraeli wa kiume wenye
umri wa miaka 20 na zaidi
wanaandikishwa kwa ajili ya jeshi
isipokuwa Walawi.
Walawi wanawekwa kando ili kuwasaidia makuhani.
Sura ya 5 hadi ya 9
zinazungumzia uaminifu katika ndoa,
kuwatenga wagonjwa
na utumishi wa wanadhiri.
Katika sura ya 10, Waisraeli
wanaondoka katika nyika ya Sinai
kulingana na mgawanyo wa makabila yao.
Katika sura ya 11,
watu wanalalamika kuhusu mana,
chakula kilichoandaliwa
kimuujiza na Yehova.
Katika sura inayofuata,
Miriamu na Haruni
wanasema vibaya kumhusu Musa
kwa sababu hiyo Miriamu
anapigwa na ukoma kwa muda mfupi
na anatengwa kwa siku saba.
Katika sura ya 13 na 14,
wakuu kumi na mbili wa Israeli
mmoja kutoka kila kabila
wanatumwa kuenda
kupeleleza nchi ya Kanaani.
Wapelelezi kumi wanaleta ripoti mbaya
na watu wanataka kurudi Misri
kwa sababu ya ukosefu huo
mkubwa wa imani
Waisraeli wanalazimishwa
kuzunguka nyikani kwa miaka 40
mpaka kizazi hicho chote kinapokufa.
Je, ulijua?
Yoshua na Kalebu ndio wapelelezi pekee
waliokuwa na imani katika Yehova.
Kwa hiyo, wao tu ndio wapelelezi
walioruhusiwa kuingia katika nchi ya Ahadi.
Kalebu alirithi mashamba
na majiji ya Hebroni.
Urithi wa Yoshua ulikuwa
kwenye eneo lenye milima la Efraimu
ambako alikufa akiwa na
umri wa miaka 110.
Sura ya 15 hadi 17
zinazungumzia matoleo
mbalimbali ya dhambi
kutia ndani uasi wa Kora
Dathani, Abiramu
na wale waliowaunga mkono,
na pia hukumu yao ya kifo.
Katika sura ya 21,
kwa mara nyingine watu
wanalalamika kuhusu mana.
na kusema ni ‘mkate unaochukiza.’
Mfalme Balaki wa Moabu,
anamwajiri Baalamu mwenye pupa
ambaye si Mwisraeli
ili awalaani Waisraeli.
Lakini Yehova anamfanya Balaamu
awabariki Waisraeli.
Katika sura ya 25,
watumishi wengi wa Mungu
wanafanya ngono
na wanawake wa Moabu.
Hilo linaongoza kwenye ibada ya sanamu
na Mungu anawaletea pigo
linalosababisha vifo
vya Waisraeli 24,000.
Katika sura inayofuata,
Musa anawahesabu watu
kwa mara ya pili.
Katika sura ya 27,
mabinti wa Selofehadi
wanamwambia Musa
kwamba hawana ndugu atakayerithi
mali za familia yao.
Yehova anaelekeza
kwamba katika hali kama hizo
binti ndiye angepewa pendeleo hilo.
Kisha Mungu anamwamuru Musa
apande juu ya mlima
katika eneo la Abarimu
aione nchi ya ahadi.
Kwa kuwa Musa atakufa hivi karibuni,
Yehova anamwambia
amweke rasmi Yoshua
ili awaongoze Waisraeli
kuingia nchi ya Kanaani.
Sura ya 31 hadi 36
zinazungumzia
mgawanyo wa nchi ya Kanaani
na habari nyingine
huku Waisraeli
wakijiandaa kuvuka Mto Yordani.
Unaposoma kitabu cha Hesabu,
ona jinsi Yehova
anavyowaongoza watu wake kwa subira,
ona kwa nini tunapaswa kuwatii
wale waliowekwa rasmi ili kutuongoza,
na utafakari uhitaji
wa kuwa na imani yenye nguvu
tunapokaribia kuingia
katika nchi nyingine ya ahadi
ulimwengu mpya
chini ya Ufalme wa Mungu.