00:00:01
Utangulizi wa kitabu cha Waroma.00:00:04
00:00:06
Kitabu cha Waroma00:00:07
00:00:07
kimewekwa kwanza katika orodha ya barua 2100:00:10
00:00:10
za Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. 00:00:13
00:00:13
Mtume Paulo aliandika barua 14 kati ya hizo,00:00:16
00:00:16
kutia ndani Waroma.00:00:18
00:00:20
Huenda Paulo alianza safari yake ya tatu ya umishonari00:00:24
00:00:24
katika mwaka wa 52 W.K.00:00:27
00:00:28
Alipokuwa Korintho katika mwaka wa 56 W.K.,00:00:32
00:00:32
Paulo aliwaandikia Wakristo waliokuwa Roma,00:00:35
00:00:35
jiji ambalo kufikia wakati huo hakuwa amelitembelea.00:00:39
00:00:40
Barua kwa Waroma ina sura 16.00:00:43
00:00:44
Katika sura ya 1,00:00:46
00:00:46
Paulo anaelezea tamaa yake ya kuwatembelea Wakristo wanaoishi Roma00:00:50
00:00:50
ili waweze kutiana moyo.00:00:53
00:00:54
Pia anaeleza kwamba mwenendo wa ulimwengu usiompendeza Mungu00:00:58
00:00:58
hauwezi kutetewa kwa sababu sifa za Mungu zisizoonekana00:01:03
00:01:03
zinaonekana kupitia kazi zake za uumbaji.00:01:06
00:01:08
Je, ulijua? 00:01:10
00:01:10
Paulo alimtumia Tertio kuandika barua hii. 00:01:14
00:01:14
Huenda dada mwaminifu anayeitwa Fibi00:01:17
00:01:17
ndiye aliyeipeleka barua hii kule Roma00:01:19
00:01:19
au aliandamana na yule aliyeipeleka.00:01:22
00:01:23
Katika sura ya 2,00:01:24
00:01:24
Paulo anakazia kwamba Mungu hana ubaguzi.00:01:28
00:01:28
Wayahudi na Watu wa Mataifa watahukumiwa00:01:31
00:01:31
kwa kutegemea kiwango kilekile.00:01:33
00:01:34
Katika sura ya 3 na ya 4,00:01:36
00:01:36
Paulo anaeleza kwamba Yehova00:01:38
00:01:38
anawatangaza Wayahudi na Wagiriki kuwa waadilifu kwa msingi wa imani,00:01:43
00:01:43
na anatumia mfano wa Abrahamu kuonyesha jambo hilo.00:01:46
00:01:47
Abrahamu aliishi kabla ya Musa kupewa Sheria00:01:50
00:01:50
na kabla ya Yesu kudhabihu uhai wake.00:01:53
00:01:53
Hata hivyo, Mungu alimwona Abrahamu kuwa mwadilifu00:01:57
00:01:57
kwa sababu ya imani yake ya pekee.00:02:00
00:02:00
Katika sura ya 5 na ya 6,00:02:03
00:02:03
Paulo anaeleza jinsi Adamu alivyotenda dhambi dhidi ya Mungu00:02:07
00:02:07
na kwa sababu hiyo wanadamu wote wamerithi dhambi na kifo.00:02:10
00:02:11
Kitulizo kinapatikana tu kwa kuwa na imani katika Yesu00:02:15
00:02:15
na kifo chake cha kidhabihu.00:02:17
00:02:18
Katika sura ya 7 na ya 8,00:02:20
00:02:20
Paulo anaonyesha jinsi Sheria ya Musa ilivyofunua dhambi ni nini00:02:24
00:02:24
na kwa nini Wakristo hawako chini ya Sheria hiyo.00:02:28
00:02:28
Katika sura ya 9 na ya 10,00:02:30
00:02:30
Paulo anaeleza kwamba wale wanaoonyesha imani00:02:34
00:02:34
wanaweza kuwa watoto wa kiroho wa Mungu,00:02:36
00:02:36
haidhuru walizaliwa katika taifa gani.00:02:39
00:02:40
Katika sura ya 11,00:02:42
00:02:42
Paulo anatoa mfano kuhusu mzeituni.00:02:45
00:02:45
Wayahudi waliomkataa Masihi00:02:48
00:02:48
wanalinganishwa na matawi yaliyokatwa.00:02:50
00:02:51
Badala yao matawi kutoka kwenye mzeituni wa mwituni,00:02:54
00:02:54
yanayowakilisha Wakristo wasio Wayahudi,00:02:57
00:02:57
yalipandikizwa.00:02:58
00:02:59
Ili kuwa sehemu ya mti huo,00:03:01
00:03:01
kila mmoja anapaswa kuendelea kuwa mnyenyekevu00:03:04
00:03:04
na kumwamini Yesu.00:03:06
00:03:07
Katika sura ya 12 na ya 13,00:03:10
00:03:10
Paulo anawasihi Wakristo wafanye amani na watu wote,00:03:14
00:03:14
wapendane,00:03:15
00:03:15
na waheshimu mamlaka za serikali.00:03:17
00:03:18
Katika sura ya 14 na ya 15,00:03:21
00:03:21
Wakristo wanashauriwa waache kuhukumiana00:03:24
00:03:24
badala yake wawategemeze walio dhaifu.00:03:27
00:03:28
Katika sura ya 16,00:03:30
00:03:30
Paulo anamalizia kwa maneno yenye kutia moyo00:03:33
00:03:33
na kutoa salamu changamfu za kibinafsi00:03:36
00:03:36
akiwataja watu 26 kwa jina.00:03:39
00:03:41
Unaposoma barua kwa Waroma00:03:43
00:03:43
ona jinsi Mungu anavyoshughulika bila ubaguzi na watu wote,00:03:47
00:03:47
jinsi Wakristo wanavyopaswa kufanya amani na wengine,00:03:50
00:03:50
na jinsi uhuru kutoka kwa dhambi na kifo00:03:54
00:03:54
unavyowezekana tu kwa kuwa na imani katika Yesu,00:03:57
00:03:57
Mfalme wa Ufalme wa Mungu.00:04:01
Utangulizi wa Waroma
-
Utangulizi wa Waroma
Utangulizi wa kitabu cha Waroma.
Kitabu cha Waroma
kimewekwa kwanza katika orodha ya barua 21
za Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.
Mtume Paulo aliandika barua 14 kati ya hizo,
kutia ndani Waroma.
Huenda Paulo alianza safari yake ya tatu ya umishonari
katika mwaka wa 52 W.K.
Alipokuwa Korintho katika mwaka wa 56 W.K.,
Paulo aliwaandikia Wakristo waliokuwa Roma,
jiji ambalo kufikia wakati huo hakuwa amelitembelea.
Barua kwa Waroma ina sura 16.
Katika sura ya 1,
Paulo anaelezea tamaa yake ya kuwatembelea Wakristo wanaoishi Roma
ili waweze kutiana moyo.
Pia anaeleza kwamba mwenendo wa ulimwengu usiompendeza Mungu
hauwezi kutetewa kwa sababu sifa za Mungu zisizoonekana
zinaonekana kupitia kazi zake za uumbaji.
Je, ulijua?
Paulo alimtumia Tertio kuandika barua hii.
Huenda dada mwaminifu anayeitwa Fibi
ndiye aliyeipeleka barua hii kule Roma
au aliandamana na yule aliyeipeleka.
Katika sura ya 2,
Paulo anakazia kwamba Mungu hana ubaguzi.
Wayahudi na Watu wa Mataifa watahukumiwa
kwa kutegemea kiwango kilekile.
Katika sura ya 3 na ya 4,
Paulo anaeleza kwamba Yehova
anawatangaza Wayahudi na Wagiriki kuwa waadilifu kwa msingi wa imani,
na anatumia mfano wa Abrahamu kuonyesha jambo hilo.
Abrahamu aliishi kabla ya Musa kupewa Sheria
na kabla ya Yesu kudhabihu uhai wake.
Hata hivyo, Mungu alimwona Abrahamu kuwa mwadilifu
kwa sababu ya imani yake ya pekee.
Katika sura ya 5 na ya 6,
Paulo anaeleza jinsi Adamu alivyotenda dhambi dhidi ya Mungu
na kwa sababu hiyo wanadamu wote wamerithi dhambi na kifo.
Kitulizo kinapatikana tu kwa kuwa na imani katika Yesu
na kifo chake cha kidhabihu.
Katika sura ya 7 na ya 8,
Paulo anaonyesha jinsi Sheria ya Musa ilivyofunua dhambi ni nini
na kwa nini Wakristo hawako chini ya Sheria hiyo.
Katika sura ya 9 na ya 10,
Paulo anaeleza kwamba wale wanaoonyesha imani
wanaweza kuwa watoto wa kiroho wa Mungu,
haidhuru walizaliwa katika taifa gani.
Katika sura ya 11,
Paulo anatoa mfano kuhusu mzeituni.
Wayahudi waliomkataa Masihi
wanalinganishwa na matawi yaliyokatwa.
Badala yao matawi kutoka kwenye mzeituni wa mwituni,
yanayowakilisha Wakristo wasio Wayahudi,
yalipandikizwa.
Ili kuwa sehemu ya mti huo,
kila mmoja anapaswa kuendelea kuwa mnyenyekevu
na kumwamini Yesu.
Katika sura ya 12 na ya 13,
Paulo anawasihi Wakristo wafanye amani na watu wote,
wapendane,
na waheshimu mamlaka za serikali.
Katika sura ya 14 na ya 15,
Wakristo wanashauriwa waache kuhukumiana
badala yake wawategemeze walio dhaifu.
Katika sura ya 16,
Paulo anamalizia kwa maneno yenye kutia moyo
na kutoa salamu changamfu za kibinafsi
akiwataja watu 26 kwa jina.
Unaposoma barua kwa Waroma
ona jinsi Mungu anavyoshughulika bila ubaguzi na watu wote,
jinsi Wakristo wanavyopaswa kufanya amani na wengine,
na jinsi uhuru kutoka kwa dhambi na kifo
unavyowezekana tu kwa kuwa na imani katika Yesu,
Mfalme wa Ufalme wa Mungu.
-