JW subtitle extractor

Utangulizi wa Kitabu cha Waroma

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa Kitabu cha Waroma.
Waroma njo iko ku mwanzo ya barua 21 za mu Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.
Mutume Paulo aliandikaka barua 14 kati ya zile 21, kutia ndani barua kwa Waroma.
Pengine Paulo alianza safari yake ya tatu ya umisionere mu mwaka wa 52.
Wakati alikuwa Korinto,
mu mwaka wa 56,
Paulo aliandikia Wakristo wa Roma,
muji wenye alikuwa hayatembelea.
Barua yake kwa Waroma iko na sura 16.
Mu sura ya 1,
Paulo anaonyesha kama iko na hamu sana ya kuona Wakristo wa Roma
juu awatie moyo,
nao wamutie moyo.
Tena
anaonyesha kama watu wa ulimwengu hawana sababu ya kutetea mwenendo wao mubaya
juu sifa za Mungu zenye hazionekane
zinaonekana waziwazi kupitia vitu vyenye alifanya
Ulijua?
Paulo alitumia Tertio ili kuandika barua yake.
Pengine ni dada muaminifu Foibe njo aliipelekaka Roma,
ao kusindikiza wenye waliipelekaka.
Mu sura ya 2,
Paulo anaonyesha kama Mungu hana ubaguzi.
Wayahudi na Watu wa Mataifa,
wote watahukumiwa kulingana na sheria ileile.
Mu sura ya 3 na 4,
Paulo anaonyesha kama Yehova anaona Wayahudi na Wagiriki
kuwa wenye haki juu ya imani yao,
na anaonyesha vile kupitia mufano wa Abrahamu.
Abrahamu aliishi mbele Sheria ya Musa itolewe,
na mbele Yesu atoe uzima wake.
Lakini,
Mungu alimuona Abrahamu kuwa mwenye haki
kwa sababu ya imani yake kubwa.
Mu sura ya 5 na 6,
Paulo anasema kama Adamu alimukosea Mungu,
njo maana wanadamu wote wameriti zambi na kifo.
Tunaweza kutoka mu ile hali kama tu tunaonyesha imani katika Yesu na bei ya ukombozi yenye alitoa.
Mu sura ya 7 na 8,
Paulo anaonyesha namna Sheria ya Musa ilionyesha zambi ni nini
na anaonyesha juu ya nini Wakristo hawako tena chini ya Sheria.
Mu sura ya 9 na 10,
Paulo anaonyesha kama watu wa mataifa yote wenye wanaonyesha imani
wanaweza kuwa watoto wa Mungu wa kiroho.
Mu sura ya 11,
Paulo anatumia mufano wa muzeituni wenye ulipandwa.
Anafananisha Wayahudi wenye walikatala Masiya
na matawi yenye walikata.
Matawi ya muzeituni wa pori,
ni kusema Wakristo wenye hawako Wayahudi,
wanapandikizwa pa nafasi yao.
Juu wabakie ku ile muti,
wote wanapaswa kuonyesha imani katika Yesu
na kuendelea kuwa wanyenyekevu.
Mu sura ya 12 na 13,
Paulo anatia moyo Wakristo waishi kwa amani na watu wote,
wapendane,
na waheshimie wakubwa wa serikali.
Mu sura ya 14 na 15,
Paulo anashauri Wakristo waache kuhukumu wengine,
lakini,
wategemeze wazaifu.
Mu sura ya 16,
Paulo anamalizia na maneno ya kutia moyo
na anasalimia watu 26 kwa majina yao.
Wakati unasoma barua kwa Waroma yenye iliongozwa na roho,
ona namna Mungu hana ubaguzi,
namna Wakristo wanapaswa kuishi kwa amani na watu wote,
na namna tutakombolewa katika zambi na kifo
kama tu tunaonyesha imani katika Yesu,
Mufalme wa Ufalme wa Mungu.