JW subtitle extractor

Utangulizi wa 1 Wakorintho

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa Wakorintho ya Kwanza.
Mtume Paulo aliwaandikia barua hii
Wakristo waliokuwa wakiishi katika
jiji la Korintho lenye shughuli nyingi.
Paulo alikaa Korintho
wakati wa safari yake ya pili ya umishonari
na akasaidia kusitawisha kutaniko huko.
Wakati wa safari
yake ya tatu ya umishonari,
akiwa kule Efeso,
Paulo alipokea barua pamoja na habari
zenye kuhuzunisha
kuhusu kutaniko la Korintho.
Paulo aliandika barua kwa Wakorintho
mwaka wa 55 W.K. hivi
ili kushughulikia mambo hayo.
Wakorintho ya Kwanza ina sura 16.
Katika sura ya 1 hadi ya 4,
Paulo anawarekebisha Wakorintho
kwa sababu wanafikiri
kwa njia inayoleta migawanyiko
na anawasihi wawe na umoja.
Paulo anawaelewesha kwamba
si muhimu ni nani anayepanda
au kutia maji
kwa sababu Mungu ndiye anayekuza.
Katika sura ya 5 na ya 6,
Paulo anashughulikia
suala zito kuhusu uasherati.
Kuna mkosaji
asiyetubu miongoni mwao.
Mwanamume huyo anapaswa
kuondolewa ili kulilinda kutaniko.
Kutaniko
linasihiwa liukimbie uasherati.
Sura ya 7 inatoa mashauri
yenye usawaziko kuhusu useja
na kufunga ndoa.
Katika sura ya 8 hadi ya 10,
tunajifunza kwamba nyakati nyingine
tunapaswa kuepuka kufanya jambo
ambalo tuna haki ya kufanya
ili tusiwakwaze wengine
au kuzuia watu kukubali habari njema.
Je, ulijua?
Michezo ya Isthmus
ilifanyika kila baada ya miaka miwili
karibu na Korintho.
Akitumia michezo hiyo
ambayo ilifahamika vizuri,
Paulo alitoa mfano wa shindano la mbio
ili kulisaidia kutaniko la Korintho
kuelewa uhitaji wa kuwa na
uaminifu na uvumilivu.
Katika sura ya 11,
Paulo anatoa mwongozo
kuhusu Mlo wa Jioni wa Bwana.
Katika sura ya 12,
Paulo anafananisha kutaniko
na mwili wa mwanadamu
akionyesha kwamba
kila kiungo ni muhimu.
Yehova anafurahi
tunaposhirikiana kwa umoja.
Sura ya 13
inafafanua jinsi ambavyo upendo hutenda
na jinsi usivyotenda.
Sura ya 14
inaeleza kwamba mikutano ya kutaniko
inapaswa kufanywa kwa utaratibu na umoja.
Katika sura ya 15,
tunapata usadikisho kwamba
tumaini la ufufuo ni hakika.
Paulo anataja unabii uliotimizwa
na pia masimulizi ya watu
waliojionea ufufuo wa Yesu.
Anaeleza kwamba
ushindi juu ya dhambi na kifo
unapatikana kupitia
dhabihu ya fidia ya Yesu Kristo.
Katika sura ya 16,
Paulo anatoa mwongozo kuhusiana na
kukusanywa kwa michango
kwa ajili ya Wakristo wanaokabili njaa
kule Yerusalemu.
Unaposoma Wakorintho ya Kwanza,
ona jinsi Wakristo wa kweli
wanavyopaswa kuwa na umoja,
jinsi kutaniko linavyopaswa
kudumisha viwango
vya Yehova vya maadili,
na jinsi imani katika ufufuo wa Yesu
ilivyo muhimu kabisa
ikiwa tutapokea baraka za Ufalme.