JW subtitle extractor

Utangulizi wa Kitabu cha 1 Wakorinto

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa kitabu cha Wakorinto wa kwanza.
Mutume Paulo aliandikia hii barua Wakristo wa Korinto.
Korinto ilikuwa muji wenye kujaa watu wa desturi mbalimbali.
Mu safari yake ya pili ya umisionere,
Paulo alibakiaka Korinto na alisaidiaka kuanzisha kutaniko pale.
Mu safari yake ya tatu ya umisionere,
pengine wakati alikuwa Efeso,
Paulo alipataka barua kutoka kutaniko la Korinto
na pia habari ya mubaya kuhusu ile kutaniko.
Ni mu mwaka wa 55 hivi
njo Paulo aliandikiaka Wakorinto juu ya ile mambo.
Kitabu cha Wakorinto wa kwanza kiko na sura 16.
Mu sura ya 1 mupaka 4,
Paulo anashauria Wakorinto waachane na mawazo ya kuleta migawanyiko
na anawaomba wakuwe mu umoja.
Paulo anaonyesha kama
haiko mwenye anapanda ao mwenye anamwangia maji njo wa maana,
lakini Mungu mwenye anakomalishaka.
Mu sura ya 5 na 6,
Paulo anawaonyesha namna ya kushugulikia zambi nzito ya uasherati.
Mu kutaniko lao,
mulikuwa mukosaji mwenye hakutubu.
Ule mukosaji alipaswa kutengwa juu kutaniko liendelee kuwa safi.
Paulo anashauria Wakristo wa Korinto wakimbie uasherati.
Sura ya 7 iko na mashauri ya muzuri juu ya kufunga ndoa na kubakia bila kufunga ndoa.
Mu sura ya 8 mupaka 10,
tunajifunza kama wakati fulani ni muzuri kukataa kufanya jambo lenye tuko na haki ya kufanya
juu litakwaza wengine
ao litawazuia kukubali habari njema.
Ulijua?
Kila miaka mbili kulikuwa michezo ya kushindana mu rasi (isthme) ya Korinto.
Juu Wakorinto waliijua muzuri,
Paulo alitumia mufano wa watu wenye kufanya shindano la mbio
ili asaidie Wakristo wa Korinto kuelewa kama wanapaswa kuendelea kuwa waaminifu na kuvumilia.
Mu sura ya 11,
Paulo anatoa maagizo kuhusu Chakula cha Mangaribi cha Bwana.
Mu sura ya 12,
Paulo anafananisha kutaniko na mwili wa mwanadamu
na anaonyesha kama kila mutu mu kutaniko ni wa maana.
Yehova anafurahi wakati tunatumika mu umoja.
Sura ya 13 inaonyesha ni mambo gani mutu mwenye upendo anafanyaka
na ni nini hafanyake.
Sura ya 14 inaonyesha kama mikutano ya kutaniko inapaswa kufanywa kwa utaratibu na kwa amani.
Sura ya 15 inatuhakikishia kama kutakuwaka ufufuo.
Paulo anaonyesha kama ufufuo wa Yesu ulitimiza unabii wa Biblia
na kama watu mingi walionaka Yesu kisha kufufuliwa.
Anaonyesha pia kama
wanadamu watakombolewa mu zambi na kifo
kupitia bei ya ukombozi ya Yesu.
Mu sura ya 16,
Paulo anatoa maagizo kuhusu namna ya kufanya michango ya kusaidia Wakristo maskini wa Yerusalemu.
Wakati unasoma Wakorinto wa Kwanza,
ona namna Wakristo wa kweli wanapaswa kuwa mu umoja,
namna kutaniko linapaswa kufuata kanuni za Yehova za mwenendo,
na namna ufufuo wa Yesu ni wa maana sana juu tupate baraka za Ufalme.