00:00:02
Utangulizi wa Wakorintho ya Pili.00:00:04
00:00:06
Miezi kadhaa baada
ya kutaniko la Wakorintho00:00:09
00:00:09
kupokea barua ya kwanza,00:00:11
00:00:11
Paulo aliwaandikia barua
ya pili iliyoongozwa na roho.00:00:14
00:00:16
Tito alikuwa ametumwa Korintho00:00:18
00:00:18
akasaidie kukusanya michango00:00:20
00:00:20
kwa ajili ya ndugu waliokuwa Yudea00:00:22
00:00:22
na labda pia kuona jinsi ambavyo00:00:24
00:00:24
Wakorintho wangetenda baada ya00:00:25
00:00:25
kupata barua ya
kwanza iliyoongozwa na roho.00:00:28
00:00:28
Tito alipoondoka Korintho,
alisafiri kwenda kukutana na Paulo.00:00:33
00:00:33
Kwa kuwa Tito alimpa ripoti nzuri,00:00:35
00:00:35
Paulo alishangilia na
kuwaandikia Wakorintho barua nyingine.00:00:39
00:00:41
Wakorintho ya Pili ina sura 13.00:00:45
00:00:45
Katika sura ya 1,00:00:47
00:00:47
Paulo anamfafanua Yehova kuwa00:00:49
00:00:49
“Baba wa rehema nyororo
na Mungu wa faraja yote,00:00:52
00:00:52
ambaye hutufariji
katika majaribu yetu yote.”00:00:56
00:00:57
Katika sura ya 2,00:00:58
00:00:58
Paulo analihakikishia
kutaniko hilo kwamba anawapenda,00:01:02
00:01:02
kwa sababu katika barua ya kwanza00:01:04
00:01:04
alikuwa amewapa mashauri thabiti.00:01:07
00:01:07
Mkosaji ambaye alikuwa
amefukuzwa kutoka kutanikoni00:01:11
00:01:11
alikuwa sasa amebadili njia zake00:01:13
00:01:13
na alipaswa kusamehewa
na kukaribishwa tena.00:01:16
00:01:16
Katika sura ya 3,00:01:18
00:01:18
Paulo anaandika kwamba Mungu00:01:20
00:01:20
ndiye anayemstahilisha mtu
vya kutosha kuwa mhudumu.00:01:24
00:01:25
Sura ya 400:01:26
00:01:26
inafafanua huduma ya agano jipya00:01:29
00:01:29
kuwa ‘hazina katika vyombo vya udongo.’00:01:32
00:01:33
Ingawa sisi ni
wanadamu wasio wakamilifu tu,00:01:36
00:01:36
ujumbe tunaohubiri unaweza
kuleta uzima wa milele kwetu00:01:40
00:01:40
na kwa wale wanaotusikiliza.00:01:43
00:01:44
Katika sura ya 5,00:01:45
00:01:45
Paulo anasema hivi:00:01:47
00:01:47
“Upendo alio nao
Kristo hutuchochea.”00:01:50
00:01:50
Tunapoelewa jinsi Kristo00:01:52
00:01:52
alivyotuonyesha
upendo usio wa kawaida00:01:54
00:01:54
lazima tuchochewe
kuishi kwa ajili yake.00:01:57
00:01:57
Upendo wake
unatuchochea kuiga mfano wake.00:02:00
00:02:01
Sura ya 600:02:03
00:02:03
inaeleza kwamba kuwa na ushirika00:02:04
00:02:04
kati ya Mkristo wa kweli na
mtu ambaye si Mkristo wa kweli00:02:08
00:02:08
ni kufungwa nira isiyo sawa.00:02:10
00:02:10
Kufanya hivyo
kutadhuru tu imani ya Mkristo.00:02:13
00:02:16
Sura ya 700:02:17
00:02:17
inatofautisha huzuni ya kimungu
na huzuni ya ulimwengu.00:02:22
00:02:23
Huzuni ya kimungu huonekana
mtu anapoona makosa00:02:27
00:02:27
kuwa dhambi dhidi ya Mungu.00:02:29
00:02:29
Hilo humchochea kuomba msamaha00:02:31
00:02:31
na kubadili mwenendo wake mbaya.00:02:34
00:02:35
Huzuni ya ulimwengu ni tofauti.00:02:38
00:02:38
Katika kisa hiki,00:02:39
00:02:39
ingawa mtu anaweza kuhuzunika
kwamba kosa lake limefunuliwa,00:02:43
00:02:43
hana tamaa ya kupata
msamaha wa Mungu.00:02:47
00:02:49
Katika sura ya 8 na ya 9,00:02:51
00:02:51
Paulo anawatia moyo Wakorintho
wakamilishe huduma ya kutoa msaada00:02:55
00:02:55
kwa kuwasaidia akina ndugu00:02:56
00:02:56
waliokuwa wakikabili
hali ngumu kule Yudea.00:03:00
00:03:02
Je, ulijua?00:03:04
00:03:04
Neno “huduma”
ambalo Paulo alitumia00:03:06
00:03:06
kufafanua kazi ya
kuhubiri na kufundisha00:03:09
00:03:09
ndilo neno lilelile la Kigiriki00:03:10
00:03:10
alilotumia pia kuhusu
kazi ya kutoa msaada.00:03:13
00:03:13
Hivyo, kazi ya kutoa msaada00:03:15
00:03:15
ni sehemu ya utumishi mtakatifu00:03:17
00:03:17
ambao Mkristo humtolea Yehova.00:03:20
00:03:20
Katika sura ya 10 hadi ya 13,00:03:23
00:03:23
Paulo anatoa hoja zinazoonyesha00:03:25
00:03:25
kwa nini mafundisho yaliyotolewa00:03:26
00:03:26
na mitume wa uwongo si ya kweli.00:03:29
00:03:29
Paulo analikumbusha kutaniko kwamba00:03:31
00:03:31
kweli ya Kimaandiko00:03:33
00:03:33
inaweza kupindua mafundisho,00:03:35
00:03:35
mazoea, na mitazamo00:03:37
00:03:37
inayotegemea hekima ya
wanadamu wasio wakamilifu00:03:39
00:03:39
iliyo kama
“ngome zenye nguvu.”00:03:42
00:03:43
Unaposoma Wakorintho ya Pili,00:03:45
00:03:45
ona jinsi Yehova,
Mungu wa faraja yote,00:03:48
00:03:48
anavyowaimarisha na kuwategemeza
watumishi wake,00:03:52
00:03:52
jinsi msamaha wa kweli
unavyoongoza kwenye00:03:55
00:03:55
urafiki pamoja na Mungu,00:03:56
00:03:56
na jinsi hata wanadamu dhaifu00:03:59
00:03:59
wanavyoweza
kutangaza habari njema00:04:01
00:04:01
ya Ufalme wa Mungu.00:04:03
Utangulizi wa 2 Wakorintho
-
Utangulizi wa 2 Wakorintho
Utangulizi wa Wakorintho ya Pili.
Miezi kadhaa baada
ya kutaniko la Wakorintho
kupokea barua ya kwanza,
Paulo aliwaandikia barua
ya pili iliyoongozwa na roho.
Tito alikuwa ametumwa Korintho
akasaidie kukusanya michango
kwa ajili ya ndugu waliokuwa Yudea
na labda pia kuona jinsi ambavyo
Wakorintho wangetenda baada ya
kupata barua ya
kwanza iliyoongozwa na roho.
Tito alipoondoka Korintho,
alisafiri kwenda kukutana na Paulo.
Kwa kuwa Tito alimpa ripoti nzuri,
Paulo alishangilia na
kuwaandikia Wakorintho barua nyingine.
Wakorintho ya Pili ina sura 13.
Katika sura ya 1,
Paulo anamfafanua Yehova kuwa
“Baba wa rehema nyororo
na Mungu wa faraja yote,
ambaye hutufariji
katika majaribu yetu yote.”
Katika sura ya 2,
Paulo analihakikishia
kutaniko hilo kwamba anawapenda,
kwa sababu katika barua ya kwanza
alikuwa amewapa mashauri thabiti.
Mkosaji ambaye alikuwa
amefukuzwa kutoka kutanikoni
alikuwa sasa amebadili njia zake
na alipaswa kusamehewa
na kukaribishwa tena.
Katika sura ya 3,
Paulo anaandika kwamba Mungu
ndiye anayemstahilisha mtu
vya kutosha kuwa mhudumu.
Sura ya 4
inafafanua huduma ya agano jipya
kuwa ‘hazina katika vyombo vya udongo.’
Ingawa sisi ni
wanadamu wasio wakamilifu tu,
ujumbe tunaohubiri unaweza
kuleta uzima wa milele kwetu
na kwa wale wanaotusikiliza.
Katika sura ya 5,
Paulo anasema hivi:
“Upendo alio nao
Kristo hutuchochea.”
Tunapoelewa jinsi Kristo
alivyotuonyesha
upendo usio wa kawaida
lazima tuchochewe
kuishi kwa ajili yake.
Upendo wake
unatuchochea kuiga mfano wake.
Sura ya 6
inaeleza kwamba kuwa na ushirika
kati ya Mkristo wa kweli na
mtu ambaye si Mkristo wa kweli
ni kufungwa nira isiyo sawa.
Kufanya hivyo
kutadhuru tu imani ya Mkristo.
Sura ya 7
inatofautisha huzuni ya kimungu
na huzuni ya ulimwengu.
Huzuni ya kimungu huonekana
mtu anapoona makosa
kuwa dhambi dhidi ya Mungu.
Hilo humchochea kuomba msamaha
na kubadili mwenendo wake mbaya.
Huzuni ya ulimwengu ni tofauti.
Katika kisa hiki,
ingawa mtu anaweza kuhuzunika
kwamba kosa lake limefunuliwa,
hana tamaa ya kupata
msamaha wa Mungu.
Katika sura ya 8 na ya 9,
Paulo anawatia moyo Wakorintho
wakamilishe huduma ya kutoa msaada
kwa kuwasaidia akina ndugu
waliokuwa wakikabili
hali ngumu kule Yudea.
Je, ulijua?
Neno “huduma”
ambalo Paulo alitumia
kufafanua kazi ya
kuhubiri na kufundisha
ndilo neno lilelile la Kigiriki
alilotumia pia kuhusu
kazi ya kutoa msaada.
Hivyo, kazi ya kutoa msaada
ni sehemu ya utumishi mtakatifu
ambao Mkristo humtolea Yehova.
Katika sura ya 10 hadi ya 13,
Paulo anatoa hoja zinazoonyesha
kwa nini mafundisho yaliyotolewa
na mitume wa uwongo si ya kweli.
Paulo analikumbusha kutaniko kwamba
kweli ya Kimaandiko
inaweza kupindua mafundisho,
mazoea, na mitazamo
inayotegemea hekima ya
wanadamu wasio wakamilifu
iliyo kama
“ngome zenye nguvu.”
Unaposoma Wakorintho ya Pili,
ona jinsi Yehova,
Mungu wa faraja yote,
anavyowaimarisha na kuwategemeza
watumishi wake,
jinsi msamaha wa kweli
unavyoongoza kwenye
urafiki pamoja na Mungu,
na jinsi hata wanadamu dhaifu
wanavyoweza
kutangaza habari njema
ya Ufalme wa Mungu.
-