JW subtitle extractor

Utangulizi wa Kitabu cha 2 Wakorinto

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa Kitabu cha Wakorinto wa Pili
Paulo aliandikia Wakristo wa Korinto barua ya pili yenye kuongozwa na roho
miezi fulani kisha wao kupata barua yake ya kwanza.
Tito alitumwa Korinto juu ya kusaidia kukusanya feza kwa ajili ya ndugu wa Yudea
na inawezekana pia juu ya kuangalia namna Wakristo wa Korinto walitenda wakati walipata barua ya kwanza ya Paulo.
Wakati Tito alirudia, alienda kukutana na Paulo.
Paulo alifurahi juu Tito alimuletea habari ya muzuri,
na akaandikia tena Wakristo wa Korinto barua ya pili.
Kitabu cha Wakorinto wa pili kiko na sura 13.
Mu sura ya kwanza, Paulo anazungumuzia Yehova kuwa “Baba wa rehema nyingi na Mungu wa faraja yote,
mwenye anatufariji katika majaribu yetu yote.”
Mu sura ya pili, Paulo anahakikishia Wakristo wa Korinto kama anawapenda,
akifikiria mashauri makali yenye aliwatolea mu barua yake ya kwanza.
Mukosaji mwenye alitengwa na kutaniko sasa ametubu
na anapaswa kusamehewa na kukaribishwa tena mu kutaniko.
Mu sura ya tatu, Paulo anaandika kama ni Mungu njo anafanya tustahili kabisa kuwa watumishi.
Sura ya ine inazungumuzia watumishi wa agano jipya kuwa “hazina katika vyombo vya udongo.”
Hata kama tuko tu vyombo vya udongo vyenye havikamilike,
ujumbe wenye tunahubiri unaweza kutusaidia sisi na kusaidia wenye kutusikiliza kupata uzima wa milele.
Mu sura ya tano, Paulo anasema: “Upendo wenye Kristo iko nao unatulazimisha.”
Kama tunaelewa upendo mukubwa wenye Yesu alituonyesha,
itakuwa mwepesi kwetu kuishi kwa ajili yake.
Upendo wake unatuchochea kumuiga.
Sura ya sita inasema kama kushirikiana na mutu mwenye haiko Mukristo wa kweli itakuwa kufungwa nira yenye haiko sawa.
Kutafikia tu kuharibu imani ya Mukristo wa kweli.
Sura ya saba inaonyesha tofauti kati ya huzuni yenye kupatana na mapenzi ya Mungu na huzuni ya ulimwengu.
Huzuni yenye kupatana na mapenzi ya Mungu inaonekana wakati mutu anaona makosa yake kuwa zambi kwa Mungu.
Ile inamusukuma atafute musamaha na abadilike.
Huzuni ya ulimwengu iko tofauti.
Hata kama mutu anaweza kuhuzunika juu makosa yake imefunuliwa,
ile haimaanishe kama anapenda Mungu amusamehe.
Mu sura ya 8 na ya 9,
Paulo anatia moyo Wakorinto waendelee na utumishi wa kutoa musaada juu ya kusaidia ndugu wa Yudea wenye kuwa mu uhitaji.
Ulijua?
Paulo alitumia neno lilelile la Kigiriki “utumishi”
juu ya kuzungumuzia kazi ya kuhubiri na kufundisha na ya kutolea wengine misaada.
Ni kusema, kutolea wengine misaada ni sehemu ya utumishi mutakatifu.
Mu sura ya 10 mupaka 13,
Paulo anafasiria Wakorinto juu ya nini mafundisho ya mitume wa uongo ni ya mubaya.
Paulo anakumbusha kutaniko kama kweli ya Maandiko inaweza kupindua mafundisho
na matendo “yenye yametia mizizi kabisa” yenye kuonyesha hekima yenye haikamilike ya wanadamu.
Wakati unasoma Wakorinto wa pili,
ona namna Yehova, Mungu wa faraja yote, anatia nguvu watumishi wake,
namna toba ya kweli inafanya mutu akuwe na uhusiano muzuri na Mungu,
na namna wanadamu wenye ni vyombo vya udongo wanaweza kutangaza habari njema ya Ufalme wa Mungu.