JW subtitle extractor

Utangulizi wa Wagalatia

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa kitabu cha Wagalatia.
Mtume Paulo aliandika barua hii
wakati wa au baada ya
ziara yake ya pili ya umishonari,
akiwa Korintho au
akiwa Antiokia ya Siria.
Ingawa kwa kawaida alimtumia
mwandishi kuandika barua zake,
Paulo mwenyewe ndiye
aliyeandika barua kwa Wagalatia.
Barua kwa Wagalatia iliandikwa
mwaka wa 50 hadi 52 W.K. hivi.
Je, ulijua?
Galatia ulikuwa mkoa wa Roma
uliokuwa sehemu ya katikati ya eneo
linalojulikana leo kuwa Asia Ndogo.
Huenda makutaniko ya Wagalatia
ambayo Paulo aliyaandikia
yalitia ndani yale
ya Antiokia ya Pisidia,
Ikoniamu, Listra, na Derbe.
Paulo alitumia barua hii
kupinga kazi ya walimu wa uwongo
ambao walidai kwamba
kufuata Sheria ya Musa
ni sehemu muhimu
ya Ukristo wa kweli.
Barua ya Wagalatia ina sura sita.
Katika sura ya 1,
Paulo anasimulia jinsi yeye mwenyewe
alivyogeuzwa imani kutoka
dini ya Kiyahudi na kuwa Mkristo.
Anawakumbusha Wagalatia kwamba
kile ambacho aliwafundisha
kilikuja kupitia ufunuo wa Yesu Kristo
na hivyo hawapaswi kukengeuka.
Katika sura ya 2 na ya 3,
Paulo anaonyesha
kwamba “matendo ya sheria”
hayawezi kumfanya
mtu awe mwadilifu.
Anaiita Sheria “mtunzaji”
aliyewaongoza watu kwa Kristo.
Mtu anafanywa kuwa mwadilifu
kupitia kuweka imani katika Yesu.
Paulo anatambulisha uzao
wa kiroho wa Abrahamu
kuwa Kristo na wale ambao
ni warithi pamoja na Kristo.
Hata hivyo,
kwenye sura ya 4 hadi ya 6,
Paulo anaonya kwamba Wagalatia
wanakabili hatari ya kuwa watumwa
wa mafundisho ya wanadamu.
Katika sura ya 4,
Paulo anatoa utangulizi wa tukio la mfano,
akitumia mfano wa Hagari na Sara
na watoto wao, Ishmaeli na Isaka.
Hagari na Ishmaeli
wanawakilisha Yerusalemu la kidunia
lililotekwa pamoja
na watoto, au wazao wake.
Sara na Isaka wanawakilisha
“Yerusalemu la juu”
sehemu ya kimbingu ya tengenezo la Yehova
na watoto wake, watiwa-mafuta kwa roho
na wana wa Mungu wenye uhuru.
Hata hivyo,
uhuru huo haupaswi kutumiwa
kuwa sababu ya kufanya
dhambi, anaonya Paulo.
Anatofautisha kazi za mwili
na tunda la roho ya Mungu,
na anafundisha kwamba
tutavuna kile tunachopanda.
Unaposoma barua kwa Wagalatia,
ona jinsi Wakristo wanavyoweza
kutangazwa kuwa waadilifu kupitia imani,
jinsi wale wanaoonyesha tunda la roho
ya Mungu wanavyopata faida,
na jinsi uzao wa kiroho wa Abrahamu
unavyotambuliwa
kuwa Kristo Yesu
na wale warithi wenzake
wa Ufalme wa milele.