JW subtitle extractor

Utangulizi wa Waefeso

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa kitabu cha Waefeso.
Mtume Paulo alifika kwanza
katika jiji la bandarini la Efeso
wakati wa ziara
yake ya pili ya umishonari,
huenda katika mwaka wa 52 W.K.,
akiandamana na Akila na Prisila.
Baada ya ziara fupi,
Paulo aliondoka,
akiwaacha Akila na Prisila
waendelee kuhubiri na kufundisha.
Lakini wakati wa ziara yake
ya tatu ya umishonari,
Paulo alikaa kwa karibu miaka mitatu,
akitimiza huduma yake kwa bidii
na kufanyiza urafiki wa karibu
na akina ndugu Waefeso.
Baadaye, karibu mwaka
wa 60 au 61 W.K.,
mtume Paulo aliandika barua
kwa kutaniko la Efeso.
Aliiandika akiwa Roma,
alipokuwa chini ya ulinzi
akisubiri kesi yake.
Barua kwa Waefeso ina sura sita.
Sura ya 1 inakazia kwamba Mungu
alikusudia kuwe na usimamizi
(au njia ya kusimamia nyumba yake).
Kupitia njia hiyo,
wale waliochaguliwa kuishi
mbinguni na watakaoishi duniani
wataunganishwa na
Yehova kupitia Kristo.
Katika sura ya 2,
mtume analinganisha Sheria ya Musa
na ukuta ambao kwa muda mrefu
uliwatenganisha Wayahudi
na Watu wa Mataifa.
Kifo cha kidhabihu cha Yesu
kiliondoa agano la Sheria
na hivyo “kuuharibu ukuta wa katikati”
uliotenganisha vikundi hivyo viwili.
Katika sura ya 3,
Paulo anataja “siri takatifu ya Kristo”
na kueleza kwamba
ni mapenzi ya Mungu
kuwaongeza watu wasio Wayahudi
katika idadi ndogo ya wanadamu
waliochaguliwa kutawala
na Kristo mbinguni.
Je, ulijua?
Jiji la Efeso lilijulikana sana
kwa hekalu kubwa la
mungu wa kike Artemi.
Kama inavyosimuliwa
kwenye Matendo 19,
mafundi wa fedha Waefeso
walikuwa na biashara
iliyowaletea faida kubwa
ya kuuza
“vihekalu vya fedha vya Artemi.”
Alipokaa Efeso kwa miaka mitatu hivi,
Paulo alifichua uwongo wa
kutumia sanamu katika ibada.
Kwa hiyo, watu kadhaa jijini Efeso
wakaacha ibada ya
sanamu na kuwa waamini.
Kwa sababu hiyo,
waliokuwa wakitengeneza
na kuuza sanamu hizo
wakakasirika na
kusababisha mvurugo.
Katika sura ya 4,
Waefeso wanashauriwa
‘wavue utu wa zamani,’
unaopatana na mwenendo
wao wa zamani,
na ‘wavae utu mpya’ unaopatana
na mapenzi ya Yehova.
Katika sura ya 5,
Paulo anawatia moyo Waefeso
‘waendelee kutembea
katika upendo.’
Upendo huo unapaswa
kuonekana katika familia.
Wake wanashauriwa
“wajitiishe kwa waume zao.”
Waume wanashauriwa
‘waendelee kuwapenda’ wake zao,
“kama vile Kristo pia
alivyolipenda kutaniko.”
Katika sura ya 6,
Paulo anatumia mfano kuhusu silaha
na kuwasihi Waefeso wavae
mavazi kamili ya silaha za kiroho.
Kufanya hivyo
kutawasaidia waendelee kuwa
waaminifu licha ya hali ngumu.
Unaposoma barua iliyoongozwa
na roho kwa Waefeso,
ona jinsi tunavyopaswa kuvaa utu mpya
kupatana na mapenzi ya Yehova,
jinsi tunavyopaswa kuvaa mavazi
kamili ya silaha za kiroho,
na jinsi Yehova alivyokusudia
kuwaunganisha Wayahudi
na Wasio Wayahudi
kuwa warithi pamoja
na Kristo katika Ufalme.