JW subtitle extractor

Utangulizi wa Wafilipi

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa kitabu cha Wafilipi.
Mtume Paulo aliandika barua hii
iliyoongozwa na roho
akiwa Roma,
ambako alikuwa akitumikia
kifungo cha nyumbani.
Aliandika barua hiyo
mwaka wa 60 au 61 W.K.
Miaka kadhaa mapema,
katika ziara yake ya pili ya umishonari,
Paulo alikuwa amepokea
maono akiwa Troa.
Mwanamume Mmakedonia
alimsihi hivi:
“Vuka uingie Makedonia utusaidie.”
Hivyo mwaka wa 50 hivi W.K.,
Paulo na waandamani wake
walianza kuhubiri habari njema
katika jiji la Makedonia la Filipi.
Paulo alianzisha kutaniko huko,
lakini alikabili upinzani.
Yeye na Sila walipigwa kwa fimbo
na kutupwa gerezani,
ambako miguu yao
ilifungwa katika mikatale.
Paulo alirudi Filipi wakati wa
ziara yake ya tatu ya umishonari.
Barua yake kwa kutaniko hilo
inaonyesha
kifungo cha pekee cha upendo
kilichokuwepo kati yake na
akina ndugu huko Filipi.
Barua kwa Wafilipi ina sura nne.
Katika sura ya 1,
Paulo aliandika kwamba
kifungo chake jijini Roma
kilisaidia
“kuendeleza habari njema.”
Ujasiri wa mtume huyo
chini ya upinzani
uliwaimarisha ndugu wengine
kuendelea kutangaza
neno la Mungu bila woga.
Katika sura ya 2,
Paulo anawatia moyo Wafilipi
waendelee kuiga mtazamo wa Kristo.
Kisha anawapongeza Wafilipi
kwa “[kuangaza]
kama mianga katika ulimwengu.”
Je, ulijua?
Muda fulani mapema,
Wafilipi walimtuma
Epafrodito ampelekee
Paulo zawadi huko Roma.
Baadaye,
Paulo alimtuma Epafrodito
kwenda Filipi,
akamkabidhi barua yake
iliyoongozwa na roho
kwa kutaniko hilo.
Katika sura ya 3,
Paulo anaonya kuhusu wale
waliokuwa na
“uhakika katika mwili,”
inaonekana ni kwa sababu
walijivunia kuwa Wayahudi.
Paulo anasema kuwa faida zozote
alizopata akiwa Farisayo
anaziona kuwa takataka
zikilinganishwa na pendeleo
la kumjua Kristo
na kuwa katika muungano naye.
Katika sura ya 4,
Wafilipi wanakumbushwa
“[wasihangaike] kuhusiana na
jambo lolote,”
lakini wajipatie
“amani ya Mungu”
kwa kutoa sala,
dua,
na shukrani.
Pia,
Paulo analishukuru kutaniko hilo
kwa ukarimu wao wa
kumwandalia mahitaji ya kimwili.
Unaposoma barua kwa Wafilipi,
ona jinsi
kudumisha ushikamanifu tunapojaribiwa
kunavyoweza kuwatia moyo
wengine kubaki imara,
jinsi Neno la Mungu
na roho yake inavyoweza kutusaidia
kuiga mtazamo wa akili wa Kristo,
na jinsi wale wanaosali
kwa Mungu kutoka moyoni
wanavyopata amani ya kweli
huku wakiusubiri
utawala wa Ufalme wake.