JW subtitle extractor

Utangulizi wa Kumbukumbu la Torati

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa kitabu
cha Kumbukumbu la Torati.
Musa ndiye
aliyeandika Kumbukumbu la Torati
katika jangwa tambarare la Moabu
mwaka wa 1473 K.W.K.
muda mfupi kabla ya Waisraeli
kuingia nchi ya ahadi.
Jina Kumbukumbu la torati linamaanisha
“Sheria ya Pili” au “Kurudiwa kwa Sheria.”
Hata hivyo, kitabu hicho pia
ni ufafanuzi wa sheria.
Kitabu hicho kinawasihi Waisraeli
wampende na kumtii Yehova
katika nchi ambayo atawaingiza.
Kitabu hicho kimefanyizwa
hasa na hotuba nne za Musa,
wimbo wake mmoja,
na baraka ambayo aliwapa Waisraeli.
Katika hotuba ya kwanza
iliyo kwenye sura ya 1-4,
Musa anazungumzia
historia ya Waisraeli baada ya kutoka Misri,
na anawasihi watu wamkumbuke Yehova
kwa sababu ya mambo aliyowafanyia.
Kwa mfano Musa aliwakumbusha
kwamba Yehova aliangamiza
kizazi cha watu wasio waaminifu
na waoga,
ambao miaka 40 mapema,
walikuwa wamewaogopa
wakaaji wa Kanaani.
Katika hotuba ya pili
iliyo kwenye sura ya 5-26,
Musa anawahimiza watu
watii amri za Mungu,
si kama wajibu tu
bali kwa sababu wanampenda
kwa moyo,
nafsi, na nguvu zao zote.
Je, ulijua?
Nyakati za kale
mara nyingi wageni
hawakuwa na haki za kisheria
na wajane na mayatima
walikabili matatizo mengi.
Hata hivyo katika Israeli,
Sheri ya Yehova iliwahusu
na kuwanufaisha watu wote
kutia ndani
wageni, wajane, na mayatima.
Yehova anawapenda sana
na watumishi wake
wanapaswa kuwapenda pia.
Katika sura ya 7,
Musa anawaambia Waisraeli
kwamba Yehova atayaondolea mbali
mataifa yaliyo katika nchi ya ahadi
ambayo yalikuwa na watu wengi
na yenye nguvu zaidi kuliko Waisraeli.
Katika sura ya 8,
Musa anafafanua urithi wa Waisraeli
kuwa “nchi nzuri”
yenye vijito vya maji,
ngano, shayiri, mizabibu,
mitini, mikomamanga, mafuta ya zeituni,
na asali.
Lakini ni nchi iliyojaa ibada ya uongo.
Kwa hiyo katika sura ya 12,
Waisraeli wanaamriwa
wabomoe madhabahu za miungu wa uongo,
wavunjevunje nguzo zao takatifu,
wateketeze kwa moto miti yao mitakatifu
na wakatekate sanamu za kuchongwa
za miungu hiyo.
Katika sura ya 16,
Musa anawakumbusha watu wa Mungu
waendelee kusherehekea Pasaka
na kutia ndani zile sherehe
zingine tatu kuu,
sherehe ya mikate isiyo na chachu,
sherehe ya majuma
na sherehe ya vibanda.
Sura ya 18
inazungumzia nabii wa pekee
atakayetokea wakati ujao.
Musa anasema hivi:
“Yehova Mungu wenu
atawainulia nabii kama mimi
kutoka kati ya ndugu zenu.
Ni lazima mumsikilize.”
Hotuba ya tatu iliyo katika
sura ya 27 na 28
inazungumzia laana
zinazotokana na kutotii
na baraka zinazotokana na kutii.
Baada ya taifa kuvuka Mto Yordani,
laana zilipaswa kutangazwa
kuelekea Mlima Ebali
ambapo nusu ya makabila yangesimama.
Makabila yale mengine
yalipaswa kusimama
kwenye Mlima Gerizimu
na kuwabariki watu.
Hotuba ya nne ya Musa inapatikana
kwenye sura ya 29 na 30
ambapo Musa anafanya agano
pamoja na watu
na kuwaambia wachague uhai
kwa kumtii Yehova.
Katika sura ya 31,
Yehova anamweka rasmi
Yoshua achukue mahali pa Musa.
Yoshua anapaswa kuwa “jasiri na imara”
anapoliongoza taifa liingie
katika nchi ambayo Mungu amewapa.
Sura ya 32 ina wimbo wa Musa
ambapo anamsifu Yehova
kwa uaminifu wake
na kuonyesha jinsi Waisraeli
walivyokosa kuwa waaminifu.
Katika sura ya 33,
tunasoma “baraka ambayo Musa . . .
aliwatangazia Waisraeli
kabla ya kifo chake.”
Katika sura ya mwisho
Musa anapanda juu ya Mlima Nebo
ambapo anaonyeshwa nchi ya ahadi.
Yehova anamwambia:
“Nimekuruhusu uione
kwa macho yako mwenyewe,
lakini hutavuka kuingia humo.”
Kisha Musa anakufa
akiwa na umri wa miaka 120
na Yehova anamzika mahali pasipojulikana
nchini Moabu.
Unaposoma kitabu cha Kumbukumbu la Torati,
ona jinsi Yehova
anavyowabariki wanaompenda,
uone jinsi anavyowanyima
baraka wale wanaokosa kumtii
na uone jinsi
kanuni zinazofanyiza sheria ya Mungu
zinavyoonekana katika mafundisho ya Yesu
nabii aliye kama Musa
ambaye pia ndiye
Mfalme wa Ufalme wa Mungu.