00:00:01
Utangulizi wa kitabu cha Wakolosai.00:00:05
00:00:07
Mtume Paulo aliandika barua
hii iliyoongozwa na roho00:00:10
00:00:10
akiwa Roma mwaka wa 60 au 61 W.K.00:00:14
00:00:15
Wakati huo alikuwa amefungwa
gerezani kwa mara ya kwanza,00:00:18
00:00:18
akiwa katika kifungo cha nyumbani.00:00:21
00:00:21
Barua ya Paulo kwa Wakolosai inaonyesha00:00:24
00:00:24
hakuwa ametembelea eneo la Kolosai.00:00:27
00:00:27
Inaonekana kutaniko lilitokea00:00:29
00:00:29
kwa sababu ya kazi ya Epafra.00:00:31
00:00:31
Hata hivyo, Paulo aliwajua00:00:33
00:00:33
washiriki kadhaa wa kutaniko hilo,00:00:35
00:00:35
kutia ndani Afia,00:00:37
00:00:37
Arkipo,00:00:37
00:00:37
na Filemoni,00:00:38
00:00:38
ambaye pia alimwandikia barua
iliyoongozwa na roho.00:00:41
00:00:43
Muda fulani baada ya
kutaniko hilo kuanzishwa,00:00:45
00:00:46
walimu wa uwongo walijaribu00:00:47
00:00:47
kuwapotosha Wakristo
kwa falsafa za uwongo.00:00:50
00:00:52
Epafra alisafiri kilomita nyingi sana00:00:54
00:00:54
kutoka Kolosai kwenda Roma00:00:56
00:00:56
ili kumpa Paulo ripoti
kuhusu kutaniko hilo.00:00:59
00:01:01
Barua kwa Wakolosai ina sura nne.00:01:04
00:01:05
Katika sura ya 1,00:01:06
00:01:07
Paulo alieleza tamaa
yake kwamba Wakolosai00:01:09
00:01:09
waendelee kukua katika
ujuzi sahihi wa Mungu.00:01:12
00:01:13
Paulo alimfafanua Mwana wa Mungu00:01:15
00:01:15
kuwa “mfano wa Mungu asiyeonekana,00:01:18
00:01:18
mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote,”00:01:20
00:01:20
na yule ambaye kupitia kwake00:01:22
00:01:22
“vitu vingine vyote viliumbwa.”00:01:24
00:01:25
Pia, Kristo ndiye kichwa cha kutaniko.00:01:27
00:01:28
Katika sura ya 2,00:01:29
00:01:30
mtume huyo aliwaonya Wakolosai kuhusu00:01:32
00:01:32
wale wanaoeneza falsafa00:01:34
00:01:34
na umuhimu wa kushika Sheria ya Musa.00:01:36
00:01:37
Paulo anakazia kwamba00:01:38
00:01:38
Sheria ya Musa ilifutwa na kuondolewa.00:01:41
00:01:41
Kwa njia ya mfano,00:01:43
00:01:43
Mungu aliitundika kwenye
mti wa mateso wa Kristo.00:01:46
00:01:47
Je, ulijua?00:01:49
00:01:49
Kwenye Wakolosai 4:10,00:01:51
00:01:51
Paulo anamtaja “Marko,00:01:53
00:01:53
binamu ya Barnaba.”00:01:54
00:01:54
Kwa muda mfupi, Marko,00:01:56
00:01:56
ambaye pia anaitwa Yohana,00:01:58
00:01:58
aliandamana na Paulo na Barnaba00:02:00
00:02:00
katika safari yao ya
kwanza ya umishonari.00:02:02
00:02:04
Lakini Marko aliwaacha na huenda00:02:06
00:02:06
alirudi nyumbani Yerusalemu,00:02:07
00:02:07
jambo ambalo halikumfurahisha Paulo.00:02:10
00:02:11
Hata hivyo, miaka 12 baadaye,00:02:13
00:02:13
Marko alikuwa Roma
akifanya kazi na Paulo.00:02:16
00:02:16
Ni wazi kwamba00:02:17
00:02:17
tofauti yoyote kati yao
ilikuwa imetatuliwa.00:02:20
00:02:23
Katika sura ya 3,00:02:24
00:02:24
Paulo analitia moyo kutaniko00:02:26
00:02:26
“[liendelee] kutafuta mambo yaliyo juu,00:02:29
00:02:29
ambako Kristo ameketi00:02:30
00:02:30
kwenye mkono wa kuume wa Mungu.”00:02:32
00:02:34
Pia mtume aliwahimiza Wakolosai00:02:36
00:02:36
‘wauvue utu wa zamani,00:02:38
00:02:38
wajivike utu mpya,’00:02:40
00:02:40
na kuendelea “kusameheana kwa hiari.”00:02:43
00:02:46
Katika sura ya 4,00:02:47
00:02:47
Paulo anawaambia Wakolosai00:02:49
00:02:49
‘wadumu katika sala,’00:02:50
00:02:51
pamoja na kutoa shukrani.00:02:52
00:02:53
Pia aliandika hivi:00:02:55
00:02:55
“Maneno yenu na yawe
yenye neema sikuzote,00:02:58
00:02:58
yaliyokolezwa chumvi,00:03:00
00:03:00
ili mjue jinsi mnavyopaswa
kumjibu kila mtu.”00:03:03
00:03:06
Unaposoma barua iliyoongozwa
na roho kwa Wakolosai,00:03:10
00:03:10
ona jinsi tunavyopaswa kukua00:03:12
00:03:12
katika ujuzi sahihi wa Mungu,00:03:14
00:03:14
jinsi tunavyoweza kusitawisha00:03:16
00:03:16
utu kama wa Kristo,00:03:18
00:03:18
na jinsi maneno yetu yanavyopaswa00:03:20
00:03:20
kuwa yenye neema sikuzote,00:03:21
00:03:21
hasa tunapotangaza habari
njema ya Ufalme Mungu.00:03:25
Utangulizi wa Wakolosai
-
Utangulizi wa Wakolosai
Utangulizi wa kitabu cha Wakolosai.
Mtume Paulo aliandika barua
hii iliyoongozwa na roho
akiwa Roma mwaka wa 60 au 61 W.K.
Wakati huo alikuwa amefungwa
gerezani kwa mara ya kwanza,
akiwa katika kifungo cha nyumbani.
Barua ya Paulo kwa Wakolosai inaonyesha
hakuwa ametembelea eneo la Kolosai.
Inaonekana kutaniko lilitokea
kwa sababu ya kazi ya Epafra.
Hata hivyo, Paulo aliwajua
washiriki kadhaa wa kutaniko hilo,
kutia ndani Afia,
Arkipo,
na Filemoni,
ambaye pia alimwandikia barua
iliyoongozwa na roho.
Muda fulani baada ya
kutaniko hilo kuanzishwa,
walimu wa uwongo walijaribu
kuwapotosha Wakristo
kwa falsafa za uwongo.
Epafra alisafiri kilomita nyingi sana
kutoka Kolosai kwenda Roma
ili kumpa Paulo ripoti
kuhusu kutaniko hilo.
Barua kwa Wakolosai ina sura nne.
Katika sura ya 1,
Paulo alieleza tamaa
yake kwamba Wakolosai
waendelee kukua katika
ujuzi sahihi wa Mungu.
Paulo alimfafanua Mwana wa Mungu
kuwa “mfano wa Mungu asiyeonekana,
mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote,”
na yule ambaye kupitia kwake
“vitu vingine vyote viliumbwa.”
Pia, Kristo ndiye kichwa cha kutaniko.
Katika sura ya 2,
mtume huyo aliwaonya Wakolosai kuhusu
wale wanaoeneza falsafa
na umuhimu wa kushika Sheria ya Musa.
Paulo anakazia kwamba
Sheria ya Musa ilifutwa na kuondolewa.
Kwa njia ya mfano,
Mungu aliitundika kwenye
mti wa mateso wa Kristo.
Je, ulijua?
Kwenye Wakolosai 4:10,
Paulo anamtaja “Marko,
binamu ya Barnaba.”
Kwa muda mfupi, Marko,
ambaye pia anaitwa Yohana,
aliandamana na Paulo na Barnaba
katika safari yao ya
kwanza ya umishonari.
Lakini Marko aliwaacha na huenda
alirudi nyumbani Yerusalemu,
jambo ambalo halikumfurahisha Paulo.
Hata hivyo, miaka 12 baadaye,
Marko alikuwa Roma
akifanya kazi na Paulo.
Ni wazi kwamba
tofauti yoyote kati yao
ilikuwa imetatuliwa.
Katika sura ya 3,
Paulo analitia moyo kutaniko
“[liendelee] kutafuta mambo yaliyo juu,
ambako Kristo ameketi
kwenye mkono wa kuume wa Mungu.”
Pia mtume aliwahimiza Wakolosai
‘wauvue utu wa zamani,
wajivike utu mpya,’
na kuendelea “kusameheana kwa hiari.”
Katika sura ya 4,
Paulo anawaambia Wakolosai
‘wadumu katika sala,’
pamoja na kutoa shukrani.
Pia aliandika hivi:
“Maneno yenu na yawe
yenye neema sikuzote,
yaliyokolezwa chumvi,
ili mjue jinsi mnavyopaswa
kumjibu kila mtu.”
Unaposoma barua iliyoongozwa
na roho kwa Wakolosai,
ona jinsi tunavyopaswa kukua
katika ujuzi sahihi wa Mungu,
jinsi tunavyoweza kusitawisha
utu kama wa Kristo,
na jinsi maneno yetu yanavyopaswa
kuwa yenye neema sikuzote,
hasa tunapotangaza habari
njema ya Ufalme Mungu.
-