JW subtitle extractor

Utangulizi wa 2 Wathesalonike

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa
2 Wathesalonike.
Mtume Paulo aliongozwa
na roho kuandika
barua hii yenye uzito
akiwa Korintho yapata
mwaka wa 51 W.K.,
muda mfupi baada ya
kuandika barua yake ya
kwanza kwa Wathesalonike.
Katika barua ya kwanza,
Paulo aliwatia moyo
akina ndugu waishi kwa utulivu,
wafuatilie mambo yao wenyewe,
na wafanye kazi kwa bidii
ili wajitegemeze kimwili.
Shauri hilo bado lilifaa.
Inaonekana kwamba
wengine bado walikuwa
wakiingilia mambo ya wengine
na hawakutaka kufanya
kazi ili kujitegemeza.
Pia, huenda kutaniko
lilipokea barua au
jumbe ambazo
zilionekana kuwa
zilitoka kwa mtume Paulo
au ndugu wengine
wenye madaraka,
zilizosema “siku
ya Yehova imefika.”
Barua ya pili kwa
Wathesalonike
ina sura tatu.
Katika sura ya 1,
Paulo anawapongeza
akina ndugu kwa imani
na uvumilivu wao,
na anaeleza kwamba
wale walio na dhiki
watapata kitulizo
wakati ambapo Kristo
aliyetukuzwa
atakuja
akiwa na mamlaka ya
Ufalme kuwaangamiza
maadui wa Mungu.
Katika sura ya 2,
barua ya Paulo inaeleza
kwamba mambo fulani
lazima yatukie kabla
siku ya Yehova haijafika.
Mambo hayo yanatia
ndani kutokea kwa
ule uasi-imani mkubwa
na kufunuliwa kwa
“yule mtu wa uasi-sheria,”
yaani,
kikundi cha viongozi
wa kidini waasi-imani.
Mtu huyo wa mfano
angejikweza juu ya
makutaniko yote.
Je, ulijua?
Barua fulani ilisambazwa
ambayo ilisemekana
kwa uwongo kuwa
iliandikwa na Paulo.
Kwa sababu hiyo,
Paulo aliandika hivi:
“Hii ni salamu yangu,
mimi Paulo,
kwa mkono wangu
mwenyewe,
ambayo ni
ishara katika kila barua;
hivi ndivyo ninavyoandika.”
Katika sura ya 3,
Paulo analishauri
kutaniko ‘liwatie alama,’
au liache kushirikiana
na watu wowote ambao
‘hawakufuata utaratibu,’
huenda kwa kuwa
hawakutaka kufanya kazi.
Hata hivyo,
kutaniko halikupaswa
kuwaona kuwa maadui
bali walipaswa
kuwaonya
kama ndugu.
Kusudi ni kuwachochea
wafikie toba.
Unaposoma 2 Wathesalonike,
ona jinsi Shetani
anavyoweza kutumia
watu waovu,
wenye kiburi ili
kupotosha mafundisho
safi ya Kristo;
jinsi ni jambo la
hekima kwetu kuacha
kushirikiana na wale
wasio na utaratibu,
huku tukiwaonya
kama ndugu;
na jinsi tunavyohitaji
kuvumilia dhiki
huku tukingoja kwa
subira utawala wa Ufalme.