JW subtitle extractor

Utangulizi wa 1 Timotheo

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa 1 Timotheo.
Mtume Paulo aliandika
barua ya kwanza kwa Timotheo
akiwa Makedonia
yapata mwaka wa 61 hadi 64 W.K.
Paulo anaonyesha
kwamba wakati huo
Timotheo alikuwa Efeso.
Paulo aliandika 1 Timotheo ili
kuweka miongozo
ya kitengenezo
katika kutaniko na kuonya dhidi
ya mafundisho ya
uwongo na
kupenda pesa.
1 Timotheo ina sura sita.
Katika sura ya 1,
Paulo anamtia moyo
Timotheo abaki Efeso
ili awarekebishe wale
ambao wameacha kufuata
mafundisho ya Kristo.
Vilevile, Paulo anatoa
shukrani kwa ajili ya
rehema nyingi za Kristo.
Ingawa Paulo alikuwa
amelitesa kutaniko
la Kikristo,
Yesu alimwona kuwa
mwaminifu kwa kumpa huduma.
Katika sura ya 2,
Paulo anataja
uhitaji wa kusali
kwa ajili ya wengine,
kutia ndani maofisa wa serikali,
ili watu wa Mungu
waendelee kuishi
kwa utulivu na kutimiza
huduma yao kwa amani.
Anaeleza kwamba
ni mapenzi
ya Mungu “watu
wa namna zote
waokolewe na kupata ujuzi
sahihi wa kweli.”
Katika sura ya 3,
Paulo anaorodhesha
sifa za kiroho
ambazo wale wanaojitahidi
kufikia kuwa waangalizi au
watumishi wa huduma
wanapaswa kutimiza.
Je, ulijua?
Kitenzi cha Kigiriki
kinachotafsiriwa
“kujitahidi kufikia”
kinamaanisha
“kujinyoosha ili
kushika kitu fulani.”
Kwa hiyo, mtume Paulo
anaonyesha kwamba akina
ndugu wanaotaka
kuwatumikia wengine
kutanikoni wanapaswa
kujitoa kikamili.
Katika sura ya 4
Paulo anaandika
kwamba kuna kipindi
ambacho baadhi ya
Wakristo wataanguka
kutoka kwenye imani
na kujaribu
kupotosha wengine.
Waasi-imani hao
watasema uwongo
na hata kuwazuia
watu wasifunge ndoa.
Anamtia moyo
Timotheo awe mfano
mfano mzuri katika kusema,
katika mwenendo,
na katika upendo.
Timotheo anapaswa
kuendelea kujitahidi
kusoma mbele ya
watu na kufundisha.
Katika sura ya 5,
Paulo anamshauri
Timotheo awatendee
wanaume wazee kama baba,
wanaume vijana kama ndugu,
wanawake wazee kama mama,
na wanawake vijana kama dada.
Anamweleza Timotheo
kwamba ikihitajika,
makutaniko yanapaswa
kuwaandalia msaada
wa kimwili wajane
waliozeeka ambao
ambao wana uhitaji wa kweli
na wanaojulikana kwa kutenda mema.
Katika sura ya 6,
mtume Paulo anataja
kwamba wale wanaofundisha
kinyume na mafundisho ya Kristo
‘wanajivuna kwa kiburi.’
Vilevile, Paulo anataja
kwamba wale ambao
“wameazimia kuwa matajiri
huanguka kwenye
majaribu, na mtego”
na tamaa nyingi zenye madhara.
Kwa sababu ya kupenda pesa
watapata madhara ya kiroho
na maumivu mengi.
Badala ya kuwa na pupa,
wafuasi wa Kristo wanapaswa kuwa
wakarimu na tayari kushiriki
vitu vyao na wengine,
wakimtegemea Mungu,
ili waushike imara
uzima ulio wa kweli.
Unaposoma 1 Timotheo,
ona jinsi Yehova anavyotaka watu
wa namna zote waokolewe na
kupata ujuzi sahihi wa kweli,
jinsi Wakristo wanavyoweza
kuepuka kupenda pesa,
na jinsi tunavyoweza kuushika
imara uzima ulio wa kweli,
ambao tunaweza kuupata tu
kupitia Ufalme wa Mungu.