JW subtitle extractor

Utangulizi wa Yakobo

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa barua ya Yakobo.
Kuna uthibitisho wenye nguvu
kwamba Yakobo aliyeandika
barua hii iliyoongozwa na roho
alikuwa ndugu wa kambo wa Yesu.
Yakobo aliandika barua hiyo
kabla ya mwaka wa 62 W.K.
Wakati huo alikuwa
akiishi Yerusalemu.
Barua hiyo inakazia uhitaji wa
kuonyesha imani na uvumilivu
licha ya majaribu,
na kuepuka dhambi
zinazoongoza kwenye
kupoteza kibali cha Mungu,
na kuthibitisha imani yetu
kwa matendo.
Kama Yesu,
Yakobo alitumia
mifano mingi rahisi
lakini yenye nguvu
kutokana na vitu vya kawaida,
kama vile,
mawimbi ya bahari,
maua,
miti,
mtu anayejiangalia kwenye kioo,
na utajiri unaoharibika.
Barua ya Yakobo ina sura tano.
Sura ya 1
inatukumbusha ‘tuendelee
kumwomba Mungu’ hekima,
tukifanya hivyo kwa imani,
na kwamba mtu
“aliye na shaka ni
kama wimbi la bahari
linaloendeshwa na upepo
na kupeperushwa huku na huku.”
Sura ya 2
ina mashauri ya moja kwa moja kwa
wale wanaowapendelea matajiri
na kuwabagua maskini,
na hivyo kutokeza matabaka na
kuvunja “ile sheria ya kifalme”
ya kumpenda jirani.
Je, ulijua?
Yakobo anayarejelea
Mahubiri ya Mlimani mara nyingi.
Kwa mfano, anasema kwamba
tunaweza kuwa na shangwe
tunapoteswa;
tunapaswa kufanya
mapenzi ya Mungu,
si kuyasikia tu;
na ikiwa tunataka Mungu atusamehe,
lazima tuwasamehe wengine.
Katika sura ya 3,
Yakobo analinganisha
mambo kadhaa
kuonyesha kwa nini tunahitaji
kudhibiti ulimi wetu.
Hilo ni kweli
hasa kwa walimu wa
Neno la Mungu.
Yakobo analinganisha ulimi
na vitu kama vile
lijamu ya farasi,
mtambo wa usukani,
moto,
na chemchemi ya maji.
Sura ya 4
inaeleza kwamba chanzo
cha mwenendo mpotovu
ni tamaa za mwili.
Yakobo anasema hivi pia:
“Yeyote anayetaka
kuwa rafiki ya ulimwengu
anajifanya kuwa adui ya Mungu.”
Kwa upande mwingine,
tunaweza kumpinga Ibilisi
na kumkaribia Mungu,
naye atatukaribia.
Sura ya 5 inatuambia
kwamba Yehova atawaadhibu
matajiri na watu wenye uwezo
ambao huwakandamiza wengine.
Pia, Yakobo anakazia
umuhimu wa kuwa na subira.
Kama vile mkulima
anavyosubiri mvua,
tunapaswa kuwa na subira
hadi Mungu atakapotimiza
ahadi zake kupitia Kristo.
Kwa sasa, yeyote anayekuwa
mgonjwa kiroho,
anapaswa kutafuta msaada
kutoka kwa wazee wa kutaniko.
Kwa upendo,
wazee watatumia
Neno la Mungu na
sala zao za imani zinaweza
kumsaidia mgonjwa apone.
Unaposoma barua ya Yakobo,
ona kwa nini hatupaswi
kumlaumu Yehova
kwa majaribu yetu,
jinsi tunavyopaswa
kudhibiti ulimi wetu,
na jinsi tunavyopaswa
kuwa na subira
tunapoungojea Ufalme
wa Mungu.