00:00:02
Utangulizi wa barua ya Yakobo.00:00:05
00:00:07
Kuna uthibitisho wenye nguvu00:00:09
00:00:09
kwamba Yakobo aliyeandika00:00:10
00:00:10
barua hii iliyoongozwa na roho00:00:12
00:00:12
alikuwa ndugu wa kambo wa Yesu.00:00:15
00:00:15
Yakobo aliandika barua hiyo00:00:17
00:00:17
kabla ya mwaka wa 62 W.K.00:00:20
00:00:20
Wakati huo alikuwa00:00:21
00:00:21
akiishi Yerusalemu.00:00:22
00:00:24
Barua hiyo inakazia uhitaji wa00:00:26
00:00:26
kuonyesha imani na uvumilivu00:00:28
00:00:28
licha ya majaribu,00:00:29
00:00:29
na kuepuka dhambi00:00:30
00:00:30
zinazoongoza kwenye00:00:32
00:00:32
kupoteza kibali cha Mungu,00:00:33
00:00:33
na kuthibitisha imani yetu00:00:35
00:00:35
kwa matendo.00:00:36
00:00:37
Kama Yesu,00:00:38
00:00:38
Yakobo alitumia00:00:40
00:00:40
mifano mingi rahisi00:00:41
00:00:41
lakini yenye nguvu00:00:43
00:00:43
kutokana na vitu vya kawaida,00:00:45
00:00:45
kama vile,00:00:46
00:00:46
mawimbi ya bahari,00:00:47
00:00:48
maua,00:00:49
00:00:49
miti,00:00:50
00:00:50
mtu anayejiangalia kwenye kioo,00:00:52
00:00:53
na utajiri unaoharibika.00:00:55
00:00:57
Barua ya Yakobo ina sura tano.00:01:00
00:01:01
Sura ya 100:01:02
00:01:02
inatukumbusha ‘tuendelee00:01:04
00:01:04
kumwomba Mungu’ hekima,00:01:05
00:01:05
tukifanya hivyo kwa imani,00:01:07
00:01:07
na kwamba mtu00:01:08
00:01:08
“aliye na shaka ni00:01:09
00:01:09
kama wimbi la bahari00:01:10
00:01:10
linaloendeshwa na upepo00:01:12
00:01:12
na kupeperushwa huku na huku.”00:01:14
00:01:15
Sura ya 200:01:16
00:01:16
ina mashauri ya moja kwa moja kwa00:01:18
00:01:18
wale wanaowapendelea matajiri00:01:20
00:01:20
na kuwabagua maskini,00:01:21
00:01:21
na hivyo kutokeza matabaka na00:01:23
00:01:23
kuvunja “ile sheria ya kifalme”00:01:25
00:01:25
ya kumpenda jirani.00:01:27
00:01:28
Je, ulijua?00:01:30
00:01:31
Yakobo anayarejelea00:01:32
00:01:32
Mahubiri ya Mlimani mara nyingi.00:01:34
00:01:34
Kwa mfano, anasema kwamba00:01:36
00:01:36
tunaweza kuwa na shangwe00:01:37
00:01:37
tunapoteswa;00:01:38
00:01:39
tunapaswa kufanya00:01:40
00:01:40
mapenzi ya Mungu,00:01:41
00:01:41
si kuyasikia tu;00:01:43
00:01:43
na ikiwa tunataka Mungu atusamehe,00:01:45
00:01:45
lazima tuwasamehe wengine.00:01:47
00:01:49
Katika sura ya 3,00:01:51
00:01:51
Yakobo analinganisha00:01:52
00:01:52
mambo kadhaa00:01:53
00:01:54
kuonyesha kwa nini tunahitaji00:01:56
00:01:56
kudhibiti ulimi wetu.00:01:57
00:01:58
Hilo ni kweli00:01:59
00:01:59
hasa kwa walimu wa
Neno la Mungu.00:02:01
00:02:02
Yakobo analinganisha ulimi00:02:04
00:02:04
na vitu kama vile00:02:05
00:02:05
lijamu ya farasi,00:02:06
00:02:07
mtambo wa usukani,00:02:08
00:02:08
moto,00:02:10
00:02:10
na chemchemi ya maji.00:02:12
00:02:12
Sura ya 400:02:14
00:02:14
inaeleza kwamba chanzo00:02:15
00:02:15
cha mwenendo mpotovu00:02:17
00:02:17
ni tamaa za mwili.00:02:19
00:02:19
Yakobo anasema hivi pia:00:02:21
00:02:21
“Yeyote anayetaka00:02:23
00:02:23
kuwa rafiki ya ulimwengu00:02:25
00:02:25
anajifanya kuwa adui ya Mungu.”00:02:27
00:02:28
Kwa upande mwingine,00:02:30
00:02:30
tunaweza kumpinga Ibilisi00:02:32
00:02:32
na kumkaribia Mungu,00:02:34
00:02:34
naye atatukaribia.00:02:36
00:02:38
Sura ya 5 inatuambia00:02:40
00:02:40
kwamba Yehova atawaadhibu00:02:42
00:02:42
matajiri na watu wenye uwezo00:02:43
00:02:43
ambao huwakandamiza wengine.00:02:46
00:02:47
Pia, Yakobo anakazia00:02:49
00:02:49
umuhimu wa kuwa na subira.00:02:50
00:02:51
Kama vile mkulima00:02:52
00:02:52
anavyosubiri mvua,00:02:53
00:02:53
tunapaswa kuwa na subira00:02:55
00:02:55
hadi Mungu atakapotimiza00:02:56
00:02:56
ahadi zake kupitia Kristo.00:02:58
00:03:00
Kwa sasa, yeyote anayekuwa00:03:02
00:03:02
mgonjwa kiroho,00:03:04
00:03:04
anapaswa kutafuta msaada00:03:05
00:03:05
kutoka kwa wazee wa kutaniko.00:03:07
00:03:08
Kwa upendo,00:03:09
00:03:09
wazee watatumia00:03:10
00:03:10
Neno la Mungu na00:03:11
00:03:11
sala zao za imani zinaweza00:03:13
00:03:13
kumsaidia mgonjwa apone.00:03:15
00:03:17
Unaposoma barua ya Yakobo,00:03:20
00:03:20
ona kwa nini hatupaswi00:03:21
00:03:21
kumlaumu Yehova00:03:22
00:03:22
kwa majaribu yetu,00:03:24
00:03:24
jinsi tunavyopaswa00:03:26
00:03:26
kudhibiti ulimi wetu,00:03:27
00:03:27
na jinsi tunavyopaswa00:03:29
00:03:29
kuwa na subira00:03:30
00:03:30
tunapoungojea Ufalme
wa Mungu.00:03:33
Utangulizi wa Yakobo
-
Utangulizi wa Yakobo
Utangulizi wa barua ya Yakobo.
Kuna uthibitisho wenye nguvu
kwamba Yakobo aliyeandika
barua hii iliyoongozwa na roho
alikuwa ndugu wa kambo wa Yesu.
Yakobo aliandika barua hiyo
kabla ya mwaka wa 62 W.K.
Wakati huo alikuwa
akiishi Yerusalemu.
Barua hiyo inakazia uhitaji wa
kuonyesha imani na uvumilivu
licha ya majaribu,
na kuepuka dhambi
zinazoongoza kwenye
kupoteza kibali cha Mungu,
na kuthibitisha imani yetu
kwa matendo.
Kama Yesu,
Yakobo alitumia
mifano mingi rahisi
lakini yenye nguvu
kutokana na vitu vya kawaida,
kama vile,
mawimbi ya bahari,
maua,
miti,
mtu anayejiangalia kwenye kioo,
na utajiri unaoharibika.
Barua ya Yakobo ina sura tano.
Sura ya 1
inatukumbusha ‘tuendelee
kumwomba Mungu’ hekima,
tukifanya hivyo kwa imani,
na kwamba mtu
“aliye na shaka ni
kama wimbi la bahari
linaloendeshwa na upepo
na kupeperushwa huku na huku.”
Sura ya 2
ina mashauri ya moja kwa moja kwa
wale wanaowapendelea matajiri
na kuwabagua maskini,
na hivyo kutokeza matabaka na
kuvunja “ile sheria ya kifalme”
ya kumpenda jirani.
Je, ulijua?
Yakobo anayarejelea
Mahubiri ya Mlimani mara nyingi.
Kwa mfano, anasema kwamba
tunaweza kuwa na shangwe
tunapoteswa;
tunapaswa kufanya
mapenzi ya Mungu,
si kuyasikia tu;
na ikiwa tunataka Mungu atusamehe,
lazima tuwasamehe wengine.
Katika sura ya 3,
Yakobo analinganisha
mambo kadhaa
kuonyesha kwa nini tunahitaji
kudhibiti ulimi wetu.
Hilo ni kweli
hasa kwa walimu wa
Neno la Mungu.
Yakobo analinganisha ulimi
na vitu kama vile
lijamu ya farasi,
mtambo wa usukani,
moto,
na chemchemi ya maji.
Sura ya 4
inaeleza kwamba chanzo
cha mwenendo mpotovu
ni tamaa za mwili.
Yakobo anasema hivi pia:
“Yeyote anayetaka
kuwa rafiki ya ulimwengu
anajifanya kuwa adui ya Mungu.”
Kwa upande mwingine,
tunaweza kumpinga Ibilisi
na kumkaribia Mungu,
naye atatukaribia.
Sura ya 5 inatuambia
kwamba Yehova atawaadhibu
matajiri na watu wenye uwezo
ambao huwakandamiza wengine.
Pia, Yakobo anakazia
umuhimu wa kuwa na subira.
Kama vile mkulima
anavyosubiri mvua,
tunapaswa kuwa na subira
hadi Mungu atakapotimiza
ahadi zake kupitia Kristo.
Kwa sasa, yeyote anayekuwa
mgonjwa kiroho,
anapaswa kutafuta msaada
kutoka kwa wazee wa kutaniko.
Kwa upendo,
wazee watatumia
Neno la Mungu na
sala zao za imani zinaweza
kumsaidia mgonjwa apone.
Unaposoma barua ya Yakobo,
ona kwa nini hatupaswi
kumlaumu Yehova
kwa majaribu yetu,
jinsi tunavyopaswa
kudhibiti ulimi wetu,
na jinsi tunavyopaswa
kuwa na subira
tunapoungojea Ufalme
wa Mungu.
-