JW subtitle extractor

Utangulizi wa 1 Petro

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa
Petro ya Kwanza.
Mtume Petro
anajitambulisha
kuwa mwandikaji wa
barua zake
mbili zilizoongozwa na
roho
yaani Petro ya kwanza
na ya pili
Petro aliandika barua yake
ya kwanza akiwa Babiloni,
kati ya mwaka wa 62 na
64 hivi W.K.
Petro alimtumia Silvano,
anayeitwa pia Sila,
kuwa mwandishi wake.
Inawezekana kwamba
Silvano ndiye Sila ambaye
hapo awali alishirikiana
na Paulo.
Petro alielekeza barua
yake ya
kwanza kwa Wakristo
watiwa mafuta huko
Ponto, Galatia, Kapadokia,
Asia, na Bithinia.
Wakristo katika maeneo
hayo walikabili majaribu
mengi.
Barua ya kwanza ya Petro
ina sura tano.
Katika sura ya kwanza,
Petro anawakumbusha
ndugu zake watiwa-mafuta
kuhusu kuzaliwa kwao upya
“kwenye tumaini lililo hai”
linalotegemea ufufuo wa
Yesu Kristo.
Wakiendelea kuwa waaminifu,
watapata tuzo la urithi usiofifia
lililowekwa akiba
kwa ajili yao mbinguni.
Basi wanahitaji kukaza akili
zao kwenye
utendaji wa kiroho na
kuepuka tamaa za mwili.
Katika sura ya pili,
mtume
Petro anawaita wafuasi
wa Yesu watiwa-mafuta
kuwa “taifa takatifu”
na “ukuhani wa kifalme”
wanaoshiriki vitu pamoja
na wengine.
Katika sura ya tatu,
tunasoma kwamba wake
wanapaswa
kujitiisha kwa upendo chini
ya waume zao,
kama Sara alivyojitiisha
kwa Abrahamu.
Nao waume wanapaswa
kuwatendea wake zao
kwa heshima.
Je, ulijua?
Katika barua yake
ya kwanza,
Petro ananukuu angalau
vitabu sita vya Biblia:
Mwanzo, Kutoka,
Mambo ya Walawi,
Zaburi, Methali,
na Isaya.
Kwa kunukuu Neno la
Mungu,
Petro alimwiga Yesu na
kutuwekea mfano mzuri.
Katika sura ya nne,
Petro anakazia
umuhimu wa
kuishi kwa ajili ya
mapenzi ya Mungu
kwa kumwiga Kristo,
hata kama itamaanisha
kupitia majaribu makali.
Vilevile anasema
tunapaswa
“kukesha kuhusiana
na sala.”
Katika sura ya tano,
Petro anawasihi wazee
wenzake walichunge
kundi la Mungu
kwa unyenyekevu na
bila ubanafsi.
Kisha anawatia moyo
wote
wamtupie Mungu
mahangaiko yao yote
kwa sababu anawajali.
Unaposoma
Petro ya Kwanza,
ona jinsi tunavyopaswa
kukaza
akili zetu kwa
ajili ya utendaji,
jinsi waume na wake
wanavyopaswa kutendeana,
na jinsi tunavyopaswa
kuwa tayari
kuvumilia majaribu
tunaposubiri
ufalme wa Mungu uje.