JW subtitle extractor

Utangulizi wa Yoshua

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa kitabu cha Yoshua.
Kitabu cha Yoshua kinaitwa
kwa jina la mwandikaji wake,
Yoshua, mwana wa Nuni,
ambaye aliongoza Israeli
baada ya Musa.
Huenda kitabu hicho
kinarejelea mambo yaliyotokea
kwa zaidi ya miaka 20,
kuanzia 1473 K.W.K
na kufikia 1450 K.W.K
kitabu hicho kilipokamilishwa.
Kitabu cha Yoshua kinaweza
kugawanywa katika sehemu nne:
Kuingia kwa Waisraeli nchini Kanaani,
vita vya kuishinda nchi hiyo,
kugawa nchi
kwa makabila ya Israeli,
na ushauri wa mwisho
ambao Yoshua alitolea taifa lote.
Kitabu hicho kina masomo muhimu
kuhusu uhitaji wa kuwa na
ujasiri, imani, na utii
hasa watu wa Mungu
wanapokabili maadui wenye nguvu.
Katika sura ya 1 na ya 2,
Yehova anamwambia Yoshua
awe jasiri na imara,
Waisraeli wanajitayarisha
kuvuka Mto Yordani,
na Yoshua anawatuma
wapelelezi wawili waende Yeriko.
Wapelelezi hao wanaenda kwenye
nyumba ya Rahabu, aliyekuwa kahaba.
Akiongozwa na imani katika Yehova,
anawaficha wapelelezi hao,
na hivyo kukosa kutii amri ya Mfalme.
Katika sura ya 3 hadi ya 6,
taifa la Israeli
linavuka kimuujiza Mto Yordani
kwenye nchi kavu,
hata ingawa mto huo umefurika.
Waisraeli wanasherehekea Pasaka
na kuanza kula mazao ya nchi.
Kisha Yoshua anakutana
na mwanamume mwenye upanga.
Mwanamume huyo ni
“mkuu wa jeshi la Yehova.”
Yehova anamtumia kumweleza Yoshua
jinsi atakavyoshinda Yeriko.
Sura ya 6 hadi ya 12 inaeleza
kuhusu vita ya kuishinda nchi.
Katika sura ya 6, Yeriko linaangushwa.
Ni Rahabu tu na
“watu wa nyumba ya
baba yake” wanaookoka.
Katika sura ya 7,
Akani anafichuliwa
kwamba alikosa kutii
kwa kuchukua nyara kutoka Yeriko.
Kwa sababu hiyo anauawa
pamoja na familia yake,
ambao bila shaka
walimsaidia
kuficha dhambi yake.
Je, ulijua?
Rahabu na Akani
wanatupatia mfano mzuri na mbaya
wa jinsi ya kuonyesha imani na utii.
Ingawa Rahabu alikuwa Mkanaani
aliokolewa kwa sababu
aliwatii wapelelezi
na kuonyesha imani
yenye ujasiri katika Yehova.
Ingawa Akani alikuwa
mshiriki wa taifa la Mungu
lililowekwa wakfu,
na alijionea Yehova
akiangusha kuta za Yeriko,
aliuwawa kwa sababu
ya kutotii,
kukosa imani,
na kuwa mwenye pupa.
Katika sura ya 8,
Jiji la Ai lilishindwa
na likafanywa kuwa
“rundo la kudumu la magofu.”
Kisha Yoshua akawasomea
watu sheria ya Mungu.
Nusu ya taifa ilisimama
mbele ya Mlima Gerizimu,
na nusu ile nyingine
mbele ya Mlima Ebali.
Katika sura ya 9,
kwa ujanja Wagibeoni
wanafanya agano
pamoja na Yoshua,
na kwa sababu hiyo
anawaacha wakiwa hai.
Sura ya 10 hadi ya 12,
inarekodi baadhi ya ushindi
ambao Mungu aliwapa Waisraeli.
Mungu hata anawaangushia
Waamori mvua ya mawe makubwa
naye analifanya jua
lisimame tuli,
mpaka taifa la Israeli
“lilipolipiza kisasi
dhidi ya maadui wake.”
Katika sura ya 13 hadi 22,
Nchi ya Ahadi inagawanywa
miongoni mwa makabila
ya Waisraeli.
Hema la Ibada
linasimamishwa kule Shilo,
na Waisraeli wanachagua
majiji sita ya makimbilio
kwa ajili ya muuaji
asiyekusudia.
Katika sura ya 22,
makabila ya Rubeni, Gadi,
na nusu ya kabila la Manase
wanarudi kwenye urithi wao
mashariki ya Yordani.
Sura ya 23 na ya 24
ina ushauri wa mwisho
ambao Yoshua alitoa.
Anawaambia watu
wamwogope Yehova
na kumtumikia kwa utimilifu
na uaminifu.
Baada ya hapo, Yoshua
na Eleazari, mwana wa
Haruni, wanakufa.
Vilevile,
Waisraeli wanatimiza kiapo
cha kuzika mifupa ya Yosefu,
mwana wa Yakobo
katika Nchi ya Ahadi.
Unaposoma kitabu cha Yoshua
ona jinsi Yehova anavyowabariki
watu waaminifu na watiifu;
jinsi anavyowapigania
watu wake;
na jinsi anavyotimiza
ahadi zake zote,
na hivyo kuimarisha
imani yetu katika urithi wetu
wa wakati ujao
chini ya Ufalme wake mtukufu.