JW subtitle extractor

Utangulizi wa 3 Yohana

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa 3 Yohana.
Yohana aliandika barua yake
ya tatu
akiwa Efeso au karibu
na Efeso
katika mwaka wa 98 W.K. hivi.
Yohana aliandika barua hiyo kwa
ndugu mpendwa, anayeitwa Gayo,
jina la Kiroma ambalo lilitumiwa na
watu wengi wakati huo.
Yohana ya 3 ina mistari 14.
Gayo alijulikana kuwa mtumishi
mwaminifu wa Mungu
ambaye sikuzote aliwakaribisha
akina ndugu ambao hakuwafahamu.
Mtume Yohana anampongeza
kwa roho yake ya ukarimu.
Mtazamo wa Diotrefe
unatofautiana
kabisa na ule wa Gayo.
Diotrefe alikuwa na kawaida ya
kupinga mwongozo wa mitume
na alitaka kuwa wa kwanza
kati ya akina ndugu.
Diotrefe alikataa kuwakaribisha
akina ndugu waliowatembelea.
Hata alijaribu kuwazuia
na kuwatupa nje ya kutaniko
wale waliowaonyesha ukarimu.
Hata hivyo
Demetrio
Mkristo na rafiki wa karibu
wa Yohana
alisifiwa na wengine.
Huenda Demetrio ndiye
aliyepeleka barua
ya tatu ya Yohana.
Je, ulijua?
Kwenye 3 Yohana 6,
Gayo anaagizwa ashughulikie
safari ya akina ndugu wanaosafiri
“kwa njia inayomfaa Mungu.”
Huenda hilo linamaanisha
kuwaandalia akina ndugu
mahitaji yao kwa ajili ya safari.
Inaonekana kwamba Gayo
alifanya hivyo.
Mwishoni mwa barua yake ya
pili na ya tatu,
Yohana anaeleza kwamba
barua zake ni fupi
kwa sababu anatumaini
kuwaona ndugu zake karibuni
na kuzungumza nao uso kwa uso.
Unaposoma 3 Yohana,
ona jinsi inavyokazia
umuhimu wa ukarimu wa Kikristo,
jinsi inavyotofautisha
mtazamo wa Diotrefe wenye kiburi
na ule wa Gayo mpendwa,
na uone jinsi upendo wa
Yohana wenye kina
unavyoonyeshwa kuelekea
warithi wenzake wa Ufalme.