JW subtitle extractor

Utangulizi wa Ufunuo

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa kitabu
cha Ufunuo.
Kitabu cha Ufunuo kiliandikwa
na mtume Yohana
karibu na mwaka wa 96 W.K.
alipokuwa uhamishoni katika
kisiwa cha Patmo.
Kitabu cha Ufunuo kina
uhusiano wa karibu na
kitabu cha kwanza cha
Biblia, Mwanzo.
Kitabu cha Mwanzo
kinatuambia jinsi
Paradiso ilivyopotea;
kitabu cha Ufunuo
kinatueleza jinsi
Paradiso itakavyorudishwa.
Kitabu cha Ufunuo kina
sura 22
ambazo zimegawanywa
katika maono 16.
Katika sura ya 1 hadi ya 3,
Yohana anaambiwa
aandike ujumbe
kwa makutaniko saba,
yaani, Efeso, Smirna,
Pergamamu, Thiatira,
Sardi, Filadelfia, na Laodikia.
Katika sura ya 4 na ya 5,
Yohana anaona maono
ya Yehova akiwa
amekalia kiti chake cha
ufalme.
Mungu anampa
Mwanakondoo kitabu
cha kukunjwa kilicho na
mihuri saba.
Mwanakondoo huyo ndiye
Kristo aliyetukuzwa.
Katika sura ya 6,
Yesu anafungua mihuri sita.
Anapofungua mihuri minne
ya kwanza,
wapanda-farasi wanne wa
mfano wanapiga mwendo.
Mbio za wapanda-farasi
watatu wa mwisho
zinasababisha vita, njaa,
na kifo.
Katika sura ya 7,
Yohana anaona malaika
wanne wakizuia
pepo za uharibifu
mpaka Waisraeli wote wa kiroho
watiwe muhuri.
Pia, mtume Yohana anaona
umati mkubwa
usioweza kuhesabika
kutoka mataifa mbalimbali
ambao umetoka katika dhiki kuu.
Je, ulijua?
Kwenye Mwanzo 3:15,
Mungu alitabiri kwamba uzao
wa mwanamke wa mfano
ungeponda kichwa cha
nyoka aliyewashawishi
Adamu na Hawa wamwasi
Mungu.
Kitabu cha Ufunuo
kinafichua kwamba
huyo “nyoka wa zamani”
ni Shetani Ibilisi,
ambaye alitumia nyoka
kuwafanya
wanadamu wamwasi Mungu.
Sehemu ya kwanza ya uzao
wa mwanamke huyo wa mfano
ulithibitika kuwa Yesu Kristo,
Mfalme wa Kimasihi.
Unabii huo pia ulitabiri kwamba
wengine wangetawala
pamoja naye mbinguni.
Kitabu cha Ufunuo kinasema
kwamba watawala hao wenzi
wangekuwa 144,000.
Katika sura ya 8 na ya 9,
Mwanakondoo anafungua
muhuri wa saba.
Yohana anaona malaika saba
wakiwa na tarumbeta saba.
Milio ya tarumbeta hizo
inatangaza
hukumu za Mungu kwa
wanadamu.
Katika sura ya 10 na ya 11,
malaika mwenye nguvu
anampa Yohana
kitabu kidogo cha kukunjwa
na kumwamuru ale.
Kisha Yohana anaambiwa
apime
patakatifu pa hekalu.
Baada ya kufanya hivyo
anaona kile kinachowapata
mashahidi wawili wa Mungu.
Kisha malaika wa saba
anapiga tarumbeta yake
na sauti kubwa inatoa
tangazo hili:
“Ufalme wa ulimwengu
umekuwa Ufalme wa
Bwana wetu na wa Kristo
wake.”
Katika sura ya 12,
Yohana anaona mwana
akizaliwa na
kuchukuliwa haraka
kwenda kwa Mungu na kwenye
kiti chake cha ufalme
na pia anaona Shetani na
malaika zake
wakitupwa chini duniani.
Kisha katika sura ya 13,
Yohana anaona wanyama
wa mwituni wenye
kutisha wanaowatawala
wanadamu.
Sura ya 14 inamwonyesha
Mwanakondoo
akiwa amesimama juu ya
Mlima Sayuni
pamoja na wale 144,000.
Katika sura ya 15 na ya 16,
malaika saba wanamwaga
hasira ya Mungu duniani
wakitumia mabakuli saba
ya dhahabu.
Tunajifunza kwamba vita kuu
ya Mungu dhidi ya mataifa
itapiganwa katika eneo la
mfano linaloitwa Har-Magedoni.
Sura ya 17 na ya 18 zinamfafanua
kahaba aliyelewa anayeitwa
Babiloni Mkubwa,
ambaye ameketi juu ya mnyama
wa mwituni
mwenye rangi nyekundu.
Hata hivyo, mnyama huyo
aliye na pembe kumi
anamgeukia kahaba huyo na
kumwangamiza.
Katika sura ya 19,
Yohana anamwona Yesu akiwa
na majeshi yake
ya mbinguni wakiwaangamiza
waovu.
Maono matatu ya mwisho yaliyo
kwenye sura ya 20 hadi ya 22
yanaonyesha Shetani akitupwa
katika shimo refu lisilo
na mwisho,
ile Miaka Elfu ya Utawala
wa Kristo,
ufufuo wa kidunia,
na uharibifu wa milele wa
wanadamu na malaika waovu.
Pia Yohana anaona Yerusalemu
Jipya lenye utukufu
na “mto wa maji ya uzima,
ukitiririka kutoka katika kiti
cha ufalme cha Mungu na
cha Mwanakondoo.”
Kwenye kingo za mto huo
kuna “miti ya uzima.”
Unaposoma kitabu cha
Ufunuo,
ona jinsi utimizo kamili wa
ahadi ya Mungu
kwenye Mwanzo 3:15
unavyofafanuliwa kupitia
maono ya kinabii;
ona jinsi Mungu atakavyoondoa
uovu wote kupitia Kristo;
na jinsi mapenzi ya Yehova
yatakavyotendeka
duniani milele kama ilivyo
mbinguni,
kupitia Ufalme wa Mungu.