JW subtitle extractor

Utangulizi wa Waamuzi

Video Other languages Share text Share link Show times

Utangulizi wa kitabu cha Waamuzi
Kitabu cha Waamuzi kiliandikwa
na nabii Samweli.
Alikikamilisha katika
mwaka wa 1100 K.W.K.
Kinaonyesha mambo yaliyotokea
katika kipindi cha miaka 330 hivi
kuanzia 1450 hadi 1120 K.W.K.
Kitabu cha Waamuzi
kinazungumzia hasa mambo
ambayo Waamuzi walitimiza,
ambao Yehova aliwatumia
kuwakomboa watu wake
waliokuwa wakikandamizwa.
Katika sura ya 1,
tunasoma kwamba Waisraeli
hawakuwafukuza wapagani
wote waliokuwa wakiishi nchini.
Badala yake
waliwatumikisha baadhi yao.
Katika sura ya pili,
malaika anawaonya Waisraeli
kwamba kwa sababu
hawajamsikiliza Yehova,
watu wanaobaki katika nchi
watakuwa mtego kwao
na kuwafanya washiriki
ibada ya uwongo.
Katika sura ya 3 hadi ya 16,
tunaona maneno ya malaika
akianza kutimia,
baada ya Yoshua na watu
wengine wa kizazi chake kufa.
Katika tendo
liliojirudia mara nyingi,
Waisraeli walishiriki
ibada ya uwongo,
Yehova akawaacha wateswe
na maadui wao,
watu wakaanza
kumlilia wapate msaada
kisha Yehova akawainua
Waamuzi ambao waliwakomboa.
Waamuzi hao 12 ni Othnieli,
Ehudi,
Shamgari,
Baraka,
Gideoni,
Tola,
Yairi,
Yeftha,
Ibzani,
Eloni,
Abdoni,
na Samsoni.
Je, ulijua?
Waamuzi wanaotajwa
katika kitabu huki walikuwa
wanaume wenye
imani yenye nguvu
ambao waliwaongoza
na kuwakomboa watu wa Mungu
wakitambua kwamba Yehova ndiye
kiongozi na mkombozi wa kweli.
Lakini hawakuwa mahakimu
katika maana ya kisheria.
Katika sura ya 3,
mwamuzi Othnieli na
mwamuzi Ehudi
wanawakomboa Waisraeli
kutoka kwa wafalme wa
Mesapotamia na Moabu
waliokuwa wakiwakandamiza.
Katika sura ya 4,
nabii wa kike anayeitwa Debora,
anamwita mwanamume mwenye
imani anayeitwa Baraka.
Anamwabia kwamba
Yehova atampa
ushindi juu ya Sisera
mkuu wa jeshi la
mfalme Yabini Mkanaani
ambaye anawakandamiza Waisraeli.
Yehova alimpa
Baraka ushindi juu ya
jeshi lote la Sisera.
Hakubaki hata mtu mmoja.
Sisera mwenyewe aliuawa na
mwanamke aliyeitwa Yaeli.
Katika sura ya sita hadi ya nane,
Yehova anamtumia mwamuzi
Gideoni na wanaume 300 tu
kuongoza katika
kuwakomboa Waisraeli
kutoka kwa
Wamidiani wanaowakandamiza.
Sura ya 11 na 12,
zinazungumzia mambo
ambayo mwamuzi Yeftha alitimiza.
Kwa msaada wa Yehova
anawatiisha Waamoni ambao
pamoja na Wafilisti,
walikuwa wamewakandamiza Waisraeli
kwa miaka 18.
Sura ya 13 hadi ya
16, inazungumzia mambo
ambayo mwamuzi Samsoni alitimiza
mnadhiri ambaye Yehova
alimpa nguvu zisizo za kawaida.
Samsoni aliwaokoa Waisraeli
kutoka mikononi mwa Wafilisti.
Inaonekana matukio yanayotajwa
kwenye sura
ya 17 hadi 21 yalitokea
katika kipindi cha mapema zaidi.
Katika sura ya 17,
mwanamume Mwefraimu
anyeitwa Mika
ambaye alikuwa na
nyumba ya miungu,
anamwajiri Mlawi anayeitwa
Yonathani kuwa kuhani wake.
Hata hivyo,
Yonathani si wa familia
ya kikuhani.
Katika sura ya 18,
mamia ya wanaume wa
kabila la Dani,
waliokuwa njiani
kwenda kupigania
ardhi kwa ajili ya kabila lao,
wanafika nyumbai kwa Mika.
Wanaiba miungu yake
na kumchukua Yonathani
awe kuhani wao.
Katika sura ya 19 na 20,
wanaume wa jiji la Gibea
la kabila la Benjamini,
wanamtendea vibaya kingono
suriya wa Mlawi.
Wabenjamini wanakataa
kuwatoa wanume wenye hatia,
kwa hiyo makabila
yale mengine wanapigana
dhidi ya Wabenjamini na
karibu waliangamize
kabisa kabila hilo.
Unaposoma kitabu cha Waamuzi,
ona, madhara
yanayoweza kuwapata
wale wanao mwacha Yehova.
Jionee jinsi Yehova alivyo
Mungu mwenye rehema
watu wake wanapotubu
na kumlilia wapate msaada.
Na ujionee kwa nini tunaweza
kumtumaini Yehova,
Mwamuzi wetu mkuu
kutukomboa kutoka kwa maadui wetu wote
kupitia kwa Ufalme wake.