JW subtitle extractor

Somo la 41: Je, Tunapaswa Kusherehekea Siku za Kuzaliwa?

Video Other languages Share text Share link Show times

Baba,
Kwa nini hatusherehekei
siku za kuzaliwa?
Swali zuri.
Ungejibuje swali hilo
ikiwa ungekuwa shuleni?
Aaah
Kwa sababu Yehova hapendi?
Ndiyo.
Lakini sababu ni nini?
Je, wewe unapenda
zawadi na vitu vitamu?
Ndiyo!
Lakini unavipenda vikiwa hivi?
Sikukuu za kuzaliwa
huchanganya vitu vizuri
pamoja na vitu ambavyo Yehova hapendi.
Jinsi gani?
Zamani
watu waliamini kuwa kuna
roho nzuri na mbaya
na waliziogopa sana.
Walifikiri kupewa zawadi
na vitu vitamu
siku ambayo walizaliwa
kungewalinda.
Na kama leo
walitoa maombi kwamba
mambo mazuri tu yawapate.
Biblia inasemaje kuhusu siku za kuzaliwa?
Inataja kuzihusu
lakini haitaji mambo mazuri.
Kulikuwa na Farao wa Misri
na Herode katika siku za Yesu.
Walikuwa watawala wenye kiburi
na waliwaua watu
wakati wa sikukuu zao za kuzaliwa.
Je, unakumbuka ikiwa
Yesu alisherehekea sikukuu yake ya kuzaliwa?
Um,
Hapana.
Kweli kabisa.
Hakufanya hivyo.
Alituambia tusherehekee
siku ambayo alikufa.
Kwa sababu siku hiyo
inatupatia tumaini la kuishi milele.
Na alituambia tupeane zawadi
wakati wowote tunapotaka.
Kama . . .
Kama leo!
Mama yuko tayari.
Keki!
Yeee!