JW subtitle extractor

Somo la 43: Je, Yehova Anajibu Sala?

Video Other languages Share text Share link Show times

Vipi Sophia
Tunajua uko humo ndani
Yehova
Wafanye waache kunionea!
Mjinga
Sana
Twende zetu.
Tuondoke.
Haya watoto
Leo katika somo la . . .
Sofia!
Kwa nini umechelewa?
Samahani.
Ni . . . nilikuwa
Unione baadaye, unasikia?
Haya!
Nyamazeni
Sofia nenda ukete
Leo,
katika somo la hesabu
tutazungumzia hesabu
zinazohusu hasa kugawa.
Haya watoto,
Nimemaliza kusahihisha
mtihani mliofanya jana.
Hongera sana Sofia.
Angela
Umepata ngapi?
Kwani najali?
D+
Lakini angalau hukuanguka kabisa!
Haina shida!
Unaangalia nani wewe?
Sofia!
Pole,
sikukuona.
Ni kama hauonekani.
Ooh, nini hiki?
Tuonane kesho!
Mwangalie!
Uko sawa?
Acha nikusaidie.
Nyakati nyingine
wao hunionea pia.
Ilipendeza!
Halafu mwalimu akaniruhusu
nimbebe huyo sungura.
Lakini nilihitaji kuwa mwangalifu sana.
Kweli?
Nilimwita Fred.
Lakini sikuruhusiwa
nimbebe muda mrefu.
Sasa mimi ni mtaalamu wa sungura!
Ala! uko sawa binti yangu?
Eeh . . .
Tuonane kesho.
Niko sawa.
Sawa.
Leo tutazungumza
kuhusu jambo muhimu sana.
Sala.
Caleb,
Wewe unaweza kusali
kuhusu mambo gani?
Eeee,
ninaweza kusali kuhusu
mambo yanayonifurahisha.
Kama ndege!
Au aiskrimu nyingi sana!
Bora tu, nisiumwe na tumbo.
Na pia kumhusu Fred.
Haya, sawa.
Niambie, Caleb
tunaposala kabla ya kulala,
huwa tunasali kuhusu nini?
Tunamshukuru Yehova
kwa vitu vizuri alivyoumba,
kama
kama wanyama,
nyota,
na bahari.
Na kuhusu Ufalme wa Mungu
na kumwomba asaidie
ndugu na dada zetu.
Kweli kabisa.
Unaweza kusali
kwa ajili ya akina ndugu na dada,
na ukumbuke,
wao wanasali kwa ajili yako pia.
Tunajua kwamba
tunapoomba mambo yanayofaa,
Yehova anasikiliza.
Basi, kwa nini hajibu sala zangu?
Ooh, Sofia kuna nini?
Tafadhali tuambie.
Kuna msichana mmoja shuleni,
ambaye ananionea sana.
Ooh, jamani!
Pole binti yangu.
Usijali.
Nilisali kwa Yehova aache,
lakini ni kama hakunisikia.
Kwani nimemkasirisha Yehova?
Hapana binti yangu.
Yehova hajakukasirikia.
Labda Yehova hawezi kuniona.
Hapana.
Kuna mtu fulani katika Biblia,
Aliyehisi kama wewe unavyohisi.
Jina lake,
ni Hana.
Hana alimpenda Yehova sana.
Hee, nisubiri.
Lakini mwanamke mwingine
anayeitwa Penina,
alimwonea sana.
Inapendeza kuwaona
watoto wakicheza, sivyo?
Kumbe hata yeye alionewa?
Ndiyo.
Tuanze kula.
Sahani yako Hana.
Na hii ni yako Penina.
Alimwonea Hana wivu sana.
Acha nikalete maji.
Unafikiri wewe ni
wa pekee sana, sivyo?
Basi kwa nini Yehova
hajakubariki na watoto wowote?
Uko sawa Hana?
Mbona una huzuni sana?
Wengine hawangeweza kuelewa
kwa nini Hana
alikuwa na huzuni nyingi,
kwa sababu uchungu ulikuwa moyoni mwake.
Kwa hiyo, alizungumza na
yule tu ambaye angeelewa.
Yehova, tafadhali, niangalie!
Nikumbuke!
Tafadhali, usinisahau!
Tafadhali,
Nipe mtoto!
Ukinipa,
nitamtoa kwako maisha yake yote,
ili akutumikie.
Unafanya nini hapa?
Kwa nini umelewa?
Sijalewa.
Nina uchungu mwingi sana!
Ooh.
Nilikuwa nikimwomba Yehova anisaidie.
Nenda kwa amani.
Yehova na akupe kile ulichomwomba.
Unajua kwa nini Hana alijihisi vizuri,
hata ingawa sala yake
ilikuwa bado haijajibiwa?
Kwa nini?
Kwa sababu Hana alijua,
Yehova alisikiliza sala yake.
Wakati wowote
unaposali kwa Yehova,
anasikiliza kwa makini
naye anajua tunachohitaji
kuliko sisi wenyewe.
Lakini, anajibuje sala zetu?
Anazijibu kwa njia nyingi,
nyakati nyingine,
lazima tuwe na subira.
Kwani ana shughuli nyingi?
Hapana.
Ni kwa sababu inaweza
kuwa vigumu kwetu kutambua jibu.
Tuzungumzie wewe unaweza
kusali kuhusu nini.
Na kile ambacho utafanya
kesho shuleni ili kutenda
kupatana na sala zako.
Ninajua kwamba Angela
na wasichana wengine,
watanionea tu,
Lakini tafadhali,
nisaidie niwe kama Hana kesho.
Nisaidie niwe imara kama yeye.
Kisha akaenda kwenye hema la ibada,
Eli alikuwa huko.
Eli alikuwa kuhani mkuu.
Jamani! Ni wao wamefika,
kimbieni!
Angalieni,
nani huyu?
Angalieni kule!
Ndio wale!
Unafikiri watapigana?
Unafikiri alifanya nini?
Alimwambia nini?
Angela atashinda!
Unataka nini Angela?
Ooh, nilitaka tu kuuliza
kama una kalamu uniazime.
Unafikiri watapigana?
Sasa nifanye nini?
Yehova alisikia sala yake.
Yehova, ni mimi, Caleb.
Tafadhali msaidie Sophia.
Na tafadhali,
msaidie Sophia awe imara shuleni leo.
Walinde watoto katika kutaniko letu,
kama Caleb na Sophia.
Tafadhali walinde watoto wetu.
Wasaidie watoto wetu
walitukuze jina lako Yehova.
Tafadhali Yehova
wasaidie watoto wetu wakabiliane
na changamoto wanazopata.
Yehova,
tafadhali nisaidie.
Tunaomba ukubali sala hii
kupitia jina la Yesu,
-Amina.
-Amina.
Amina.
Unataka kulia?
Acha Angela!
Unanionea.
Na ukiendelea kunisumbua,
nitakushtaki!
Huwezi kunishtaki.
Ndiyo nitakushtaki,
huwezi kuniambia cha kufanya!
Tuondoke Zoe.
Dada yangu kiboko!
Wewe ni jasiri!
Uliwezaje kufanya hivyo?
Nilisali nipate ujasiri
na Yehova akanisaidia.
Hana akazaa mwana,
na kumwita mwana huyo, Samweli.
Kwa maana alisema,
nilimwomba kutoka kwa Yehova.
Hakuna aliye
mtakatifu kama Yehova.
Hakuna mwingine,
isipokuwa wewe.
Asante Yehova.