JW subtitle extractor

Sababu za Kuwa na Imani—Tunapaswa Kuwatendeaje Wengine?

Video Other languages Share text Share link Show times

Watu huwatendeaje
wale ambao ni tofauti nao?
Nilipokuwa shuleni,
wanafunzi wenzangu
waliamini ya kwamba
unapaswa kukubaliana na
maisha ya mtu
hata awe anaishi
maisha ya aina gani.
Mara nyingi
walimu walitusihi tukubaliane na
watu wanaofanya
ngono za aina mbalimbali.
Mwaka wangu wa mwisho
katika shule ya sekondari
mwalimu mpya alijiunga
na shule yetu,
alikua tofauti kwa sababu
alitoka mji mkuu
na mimi nilitoka
mji mdogo wa kijijini.
Alikuwa ametumia
miaka mingi katika chuo kikuu
kwa hiyo hawakuamini
kama kuna Mungu.
Kwenye mitandao ya kijamii
lilikuwa jambo la kawaida
kuona watu wakizungumzia
maisha mapotovu.
Mara nyingi niliona watu
wakiandika maelezo huko
wakishambulia maisha ya wengine.
Mwalimu huyo alikuwa ana
utu wa aina tofauti sana.
Alionekana anapenda
kuwashambulia wanafunzi
kwa kuwauliza maswali magumu.
Mara nyingi
angeuliza maswali darasani
kuhusu mambo yanayobishaniwa.
Hata nyakati nyingine
angesema wazi:
“Watu wa eneo hili
hawana akili sana.”
Bila shaka mambo kama hayo
yaliwakera wanafunzi.
Kwa hiyo walikataa kuwepo
wakati wa somo lake
au ikiwa wangekuwepo
wangekataa kuzungumza naye.
Nakumbuka wakisema
hawawezi kuzungumza na mtu
asiyemwamini Mungu.
Nakumbuka wanafunzi
wenzangu wakiniuliza:
“Si ninyi Mashahidi wa Yehova
mnawachukia mashoga?”
Wanafunzi wengi waliamini kwamba
sisi ni watu wenye
msimamo mkali
na hata hatungeshirikiana na
watu ambao
hawakubaliani na imani yetu.
Ni nini kilichokusaidia
kuwa na maoni ya Biblia?
Sikuzote wazazi wangu
walinisaidia kuwa na
maoni yenye usawaziko.
Kadiri nilivyokua,
walinisaidia kuelewa kwamba
ingawa hatukubaliani na
mwenendo wa aina fulani
hatumchukii mtu
anayefanya mambo hayo.
Nilijifunza mengi kutokana na
mfano wa mama yangu.
Alikuwa akifanya kazi saluni
na niliona jinsi alivyokuwa
mwenye fadhili kuelekea wengine
hata iwe walikuwa na
mwenendo gani wa kingono.
Nilifikiria mfano wa Yesu
jinsi alivyowaeleza
watu wote ujumbe.
Hata iwe njia yao
ya kufikiri ilikuwaje
au walikuwa na malezi gani.
Yesu alitumia muda
kuzungumza nao
iwe walikuwa nani
au wengine walifikiri nini kuwahusu.
Nilipenda andiko la Mathayo 5:45,
linalosema:
‘Yehova huangaza jua
na hunyesha mvua
juu ya watu wote.’
Ni wonyesho wa upendo wake
kuwaandalia wanachohitaji
hata iwe wao ni nani.
Nilipofikiria mfano wa Yesu
nilikumbuka maneno yake
kwenye Mathayo
ambapo anatuambia,
‘mambo mnayotaka
watu wawatendee
ninyi muwatendee hivyo.’
Hilo lilinifanya nifikirie
jinsi ninavyopaswa kumtendea
mwalimu wangu
nikamtendea kwa njia tofauti.
Kwa kweli, ikiwa
Yehova Mungu Mweza-Yote
ni mwenye fadhili,
mwema,
na anawatendea wote
kwa heshima,
kwa nini mimi nisifanye hivyo?
Na hilo linatia ndani
hata wale mwenendo wao
sikubaliani nao.
Yehova ametupatia
njia bora zaidi
ya kuwasaidia majirani wetu
kwa kuwasaidia wajifunze kumhusu.
Kumekuwa na matukio gani
kwasababu ya kutumia
kanuni za Biblia?
Hapo awali nilifanya kazi
kwenye hoteli moja
na mhudumu mmoja
alikuwa shoga,
baadhi ya wafanyakazi wenzake
walimtendea vibaya.
Kwa hiyo nilihakikisha kwamba
siwaungi mkono
badala yake nilimtendea
kama mtu wa kawaida.
Nilipata nafasi ya
kuwa na mazungumzo
na mwalimu wangu
na hata nikamsomea
mistari kadhaa.
Alivutiwa na kile ambacho
Biblia ilisema kuhusu
mambo ya kisayansi
na akasema angependa
kujifunza zaidi.
Siku moja mhudumu huyo
alinifikia
na akanishukuru kwa kumtendea
kwa njia tofauti na wengine.
Hata baadhi ya
wahudumu wengine waliniuliza
kwa nini nilitenda hivyo.
Hilo lilinipa nafasi ya
kuwaeleza kwamba mimi
hujaribu kutumia
kanuni za Biblia
maishani mwangu
kutia ndani jinsi
ninavyowatendea wengine.
Mwalimu huyo alibadilika
kwa kadiri fulani
kadiri mwaka ulivyosonga
aliniambia alivutiwa na
mwenendo wangu
kwa sababu nilizungumza naye
na wanafunzi wenzangu
hawakufanya hivyo.
Masomo yake
yakaanza kupendeza
kwa sababu alianza
kuwatendea wanafunzi vizuri.
Hatua kwa hatua,
wanafunzi wakaanza
kurudi darasani
na kufikia
mwishoni mwa mwaka huo,
hilo darasa tulilolipenda zaidi.
Ninapofikiria jinsi Yehova
anavyowatendea watu,
na jinsi anavyowapa wote
nafasi ya kujifunza kumhusu,
ninavutiwa naye hata zaidi