JW subtitle extractor

Utangulizi wa Sura ya 11

Video Other languages Share text Share link Show times

Yehova ameweka “mutumwa muaminifu na mwenye busara” kuwa mulinzi.
Zamani, mulinzi alikuwa anapiga pembe ao kutoa mulio fulani juu ya kuonya watu kama hatari iko inakuja.
Lakini mara mingi kazi ya mulinzi haikuwa tu kuonya watu.
Sasa, Yehova aliweka Ezekieli kuwa mulinzi.
Tafazali, tusome Ezekieli 33:7, na tuone Yehova anamuambia afanye nini.
“Sasa wewe, mwana wa binadamu, nimekuweka kuwa mulinzi kwa ajili ya nyumba ya Israeli,
na wakati unasikia neno kutoka katika kinywa changu unapaswa kuwaonya kutoka kwangu.”
Sura yenye mutajifunza sasa hivi mu kitabu Ibada Safi inategemea ile andiko, iko na kichwa “Nimekuweka Kuwa Mulinzi.”
Wakati mutazungumuzia hii habari, utaona jambo ingine yenye mulinzi alipaswa kufanya, na utaelewa muzuri zaidi sifa za Yehova.
Tafuta majibu ya hii maulizo: Ni nini inamuchochea Yehova aweke walinzi?
Walinzi wanatangazaka mambo gani mbili?
Na unapaswa kufanya nini juu ya kutegemeza ibada safi?
Inaweza kuwa nguvu kufanya kazi yenye Yehova ametupatia.
Lakini, ukuwe hakika kama “mutumwa muaminifu na mwenye busara” anafurahia namna unamusaidia na kumutegemeza.
Ukuwe pia hakika kama Yehova anafurahia kazi yako, uvumilivu wako, na ushikamanifu wako.
Habari yenye utajifunza itakupatia uhodari, na itakusaidia ujue jambo ya kufanya ili kutegemeza ibada safi.